HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 30, 2011

BARAZA LA WAFANYAKAZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO LAFANYIKA JIJINI DAR

Waziri wa Habari , Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi akiongea na viongozi na wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Vijana , Utamaduni na Michezo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nane wa Baraza hilo jijini Dar es Salaam na kuwataka kufanya kazi kwa bidii na kuepuka migogoro mahala pa kazi. Kutoka ni Naibu Waziri Dkt. Fenella Mukangara na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Seith Kamuhanda (kulia).
Viongozi na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo wakifuatilia kwa makini hotuba ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel Nchimbi aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa nane wa Baraza hilo jijini Dar es salaam.
Viongozi na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa katika picha ya pamoja wakiongozwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo (Katikati) Naibu waziri Dkt. Fenella Mukangara (wa pili kutoka kushoto), Katibu mkuu wa wizara Bw. Seith Kamuhanda (wa pili kulia) na Naibu katibu mkuu Bi. Sihaba Nkinga (kushoto).Picha na Aron Msigwa – MAELEZO.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad