HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, October 6, 2010

kapumzike kwa amani dada yetu leticia kaijage

Marehemu Leticia Kaijage enzi za uhai wake.
Waombolezaji wakiwa katika Msiba Tabata Segerea nyumbani kwa kaka wa marehemu.
Waombolezaji ambao baadhi yao walifanya kazi pamoja na Marehemu katika Kampuni za PR wakiwa msibani.
Jamaa na marafiki wa marehemu
Sanduku lililouhifadhi mwili wa Marehemu Leticia likiwa tayari kwa misa maalum ya kumuombea.
Waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu.

Marafiki wa marehemu,Celine Njuju na Betrice Singano walishindwa kujizua na kujikuta wakibubujikwa na machozi kwa huzuni ya kuondokewa na mwenzi wao.
waombolezaji wakibeba sanduku tayari kwa safari ya kwenda Kijiji cha Nyakigando Kata ya Kaibanja Wilaya ya Bukoba Vijijni ambako mwili wa marehemu utahifadhiwa katika nyumba yake ya Milele Oktoba 7,2010.
Mwili ukiingizwa katika gari na baadhi ya waombolezaji tayari kwa safari ya kwenda uwanja wa ndege ili kuweza kusafirisha mwili wa marehemu kwenda kijijini kwao Nyakigando Kata ya Kaibanja Wilaya ya Bukoba Vijijni kwa mazishi.
Gari likiwa tayari kuanza safari ya kuelekea Uwanja wa Ndege.
Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahala Pema Amina.picha zimepigwa na mdau Father Kidevu aliekuwepo bega kwa bega katika msiba huo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad