Mkulima amejiwa na Mwaandishi wa magazeti kumuhoji kuhusu maisha ya shambani. Mkulima huyu hawapendi Waandishi wa habari akaona vyema amchoshe katika kujibu maswali, na mambo yakawa hivi:
MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? Mweupe au Mwekundu?
MWANDISHI: Ng'ombe mweupe.
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi.
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Vilevile nyasi na viguta vya mahindi.
MWANDISHI: ahaa sawa, na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Mweupeee!!!!XXCCCZZZZHH!!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee...
MWANDISHI: na mwekundu?
MKULIMA: Vile vile namlaza na mwenzie.
MWANDISHI: Hii sehemu yote majumba mengi, wakati wa kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Woooteeee!!!! [akifuka kwa hasira]
MKULIMA: Mweupe ninamfunga kamba na kumzungusha malishoni na kumrudisha.
MWANDISHI: na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu? Mwekundu yeye ninamfunga kamba na kuzunguka nae kama mwenziwe tu.
MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma za ng'ombe wako unaniuliza mweupe au mwekundu halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa?????
MKULIMA: Kwa sababu ng'ombe mweupe ni wangu.
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Na mwekundu ni wangu vilevile.
shuwaini!
MWANDISHI: Wewe unawalisha ng'ombe chakula gani?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? Mweupe au Mwekundu?
MWANDISHI: Ng'ombe mweupe.
MKULIMA: Ninamlisha nyasi na viguta vya mahindi.
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Vilevile nyasi na viguta vya mahindi.
MWANDISHI: ahaa sawa, na sehemu ya kulala ni wapi?
MKULIMA: Ng'ombe yupi? mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Mweupeee!!!!XXCCCZZZZHH!!!!
MKULIMA: Mweupe ninamlaza bomani kulee...
MWANDISHI: na mwekundu?
MKULIMA: Vile vile namlaza na mwenzie.
MWANDISHI: Hii sehemu yote majumba mengi, wakati wa kulisha unafanyaje?
MKULIMA: Yupi mweupe au mwekundu?
MWANDISHI: Woooteeee!!!! [akifuka kwa hasira]
MKULIMA: Mweupe ninamfunga kamba na kumzungusha malishoni na kumrudisha.
MWANDISHI: na mwekundu vilevile?
MKULIMA: Mwekundu? Mwekundu yeye ninamfunga kamba na kuzunguka nae kama mwenziwe tu.
MWANDISHI: Kwanini kila mara nikikuuliza huduma za ng'ombe wako unaniuliza mweupe au mwekundu halafu inatokea kuwa kazi zao wote ni sawa?????
MKULIMA: Kwa sababu ng'ombe mweupe ni wangu.
MWANDISHI: Na mwekundu?
MKULIMA: Na mwekundu ni wangu vilevile.
shuwaini!
yani ni kama namuona mfugaji anavyojibu maswali, nimecheka sana....
ReplyDeletethanks dogo