HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 22, 2025

DC BAGAMOYO ATOA RAI KWA WAKUTUBI KUENDELEA KUHIFADHI, KULINDA TAARIFA ZA TAIFA

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Shaibu Ndemanga amewashauri wakutubi  kuhifadhi na kulinda taarifa na kumbukumbu za taifa lao hasa kwa kuzingatia taaluma yao ni muhimu katika ulimwengu wa sasa.

Ametoa ushauri huo alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 31 ya Chuo cha Ukutubi na uhifadhi Nyaraka (SLADS) yaliyofanyika wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani ambapo takribani  wanafunzi 135 wamehitimu stashahada ya Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka.

Ndemanga amesema katika ulimwengu wa sasa ambapo teknolojia imeendelea kukua kwa kasi Mkutubi ni mtu muhimu katika kuwa mlinzi wa taarifa na kumbukumbu.“Mmebeba mzigo mzito na  naamini mtaenda kuitendea haki taaluma yenu.”

Pamoja na ushauri huo kwa wahitimu hao pia ameiomba sekta ya elimu nchini kuangalia upya mitaala na Sera ya elimu ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira kwa  wakutubi.

Aidha amesisitiza kwamba umekuwepo uhitaji wa Wakutubi katika maktaba za shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vya Amali. 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Chuo SLADS na Mkurugenzi Mkuu wa TLSB Dkt. Mboni Ruzegea, ametumia nafasi hiyo kumshukuru  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipatia TLSB fedha za matumizi mengineyo na fedha za maendeleo.

“Sehemu ya fedha hizo zimeanza kutumika kuboresha miundombinu ya Chuo.Pia nitoe ombi kwa  Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Bogamoyo kuwezesha wanafunzi wa SLADS kupata nafasi za kufanya mafunzo kwa vitendo katika Wilaya hii.”

Wakati huo huo hiyo Mwakilishi wa Kamishna wa Elimu, Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia anayeshughulikia Masuala ya Maktaba na Kiswahili, Dkt. Maryam Mwinyi, amewaomba wahitimu hao kutumia elimu waliyoipata kuitumia kwa maendeleo na wasiitumie vibaya kwenda kubomoa taifa. 
Awali Kaimu Mkuu wa Chuo cha SLADS Bertha Mwaihojo, ametumia nafasi hiyo kuelezea mafanikio na changamoto zinazokikabili Chuo hicho ikiwemo kukosekana kwa kumbi za kufanyia mihadhara na uzio.














 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad