HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, March 22, 2025

TETE FOUNDATION YAGAWA MAHITAJI KWA WANAFUNZI WALIOPO KATA YA MIONO, CHALINZE -PWANI

 

TETE FOUNDATION kupitia mradi wake wa “TUNAAMINI KATIKA WEWE” wamekuwa wakigawa mahitaji/vifaa vya shule kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na wenye uhitaji maalumu kwa kuhakikisha mtoto hakosi shule mwaka mzima kwa sababu ya kutokuwa na mahitaji ya shule (Sare za shule, madaftari, Begi, viatu n.k)......
Mradi huu wa “Tunaamini katika wewe” unao dhaminiwa na Kampuni ya Reliance Insurance kwa takribani miaka mitatu sasa, umeongeza ufaulu wa watoto mashule na kupunguza utoro mashuleni
Zoezi hili la ugawaji wa mahitaji ya shule ulienda sambamba na Bonanza la Michezo lililojumuisha shule za msingi na Sekondari zilizopo katika kata ya Miono lililokuwa na dhumuni la kuwaleta watoto pamoja ili kuweza kutambuana na kushirikiana kwenye masomo ili kukuza ufaulu mashuleni

Imetolewa

Afisa Habari.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad