Akiwasilisha salamu za rambirambi kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, Mongella amesema chama kimetoa ubani wa shilingi milioni 20 kwa familia za marehemu na shilingi milioni 6 kwa majeruhi sita wanaoendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya.
Mongella ametoa pole kwa familia za marehemu na kuwataka kuwa na subira katika kipindi hiki kigumu.
Shughuli ya kuaga miili ya marehemu hao imefanyika katika Viwanja vya Soko la Uhindini, jijini Mbeya.

No comments:
Post a Comment