Na Mwandishi Wetu
MWANAMITINDO
 wa Kimataifa Millen Happiness Magese amekabidhi kitita cha Sh.milioni 
tatu kwa Mwanamitindo Elizabeth Masuka aliyeibuka mshindi wa Samia 
Fashion Festival Zanzibar mwaka 2024.
Millen Happiness Magese 
aliyekuwa Jaji Mkuu wa Samia Fashion Festival Zanzibar alikabidhi hundi 
ya fedha yenye thamani ya Sh.milioni tatu katika Hoteli ya Urban by City
 Blue iliyopo Jijini Dar es Salaam ambapo alimuandalia chakula cha usiku
 mwanamitindo huyo na fedha hizo zimetoka Kampuni ya Millen PRIVE $ Co 
kupitia Millen PRIVE Lifestyle ambayo yeye ndio  Mkurugenzi Mkuu.
Taarifa
  ya Mwanamitindo huyo Mtanzania anayeishi nchini Marekani aliyoitoa kwa
 vyombo vya habari Jijini Dar es Salaam amesema kuwa katika tamasha la 
Samia Fashion Festival Zanzibar yeye alikuwa Jaji Mkuu hivyo pamoja na 
kutangaza washindi  wa tamasha hilo, aliona umuhimu wa kuitambua kazi 
kubwa iliyofanywa na wanamitindo walishiriki usiku huo na kumtangaza 
Elizabeth Masuka kuwa Mwanamitindo bora wa tamasha hilo.
“Tunafahamu
 kulikuwa na Samia Fashion Festival Zanzibar ambalo liliandaliwa na dada
 yangu Khadija Mwanamboka na katika tukio hilo nilikuwa Jaji Mkuu ,hivyo
 baada ya kutangaza  washindi niliona  umuhimu wa kuitambua kazi kubwa 
iliyofanywa na wanamitindo walishiriki usiku huo na kumtangaza Elizabeth
 Masuka kuwa Mwanamitindo bora wa Samia Fashion Festival Zanzibar mwaka 
2024.
“Nimetoa fedha hizo Sh.milion tatu kwanza kwa kutambua 
mchango wa wanamitindo wote ambao wamefanya kazi kubwa na nzuri wakati 
wa tamasha hilo lakini fedha hizo ni katika kuwatia moyo wanamitindo 
wanaochipukia katika medani za Wanamitido na tatu nimetoa fedha hizo 
Sh.milioni tatu kwa Elizabeth Masuka kwa kutambua yeye ndio Mwanamitindo
 bora wa Samia Fashion Festival Zanzibar mwaka 2024.,amesisitiza Millen 
Happiness Magese.
Ameongeza kuwa amefurahishwa kufanyika kwa 
Samia Fashion Festival Zanzibar kwani limethibitisha nafasi na umuhimu 
wa wanamitindo nchini Tanzania lakini pia kutoa nafasi ya vijana wa 
Kitanzania kuonesha uwezo wao katika kutawala Jukwaa la wanamitindo.
Ametumia
 nafasi hiyo kukumbusha kuwa ni heshima kubwa kwake kuwa Jaji Mkuu wa 
Samia wa Fashion Festival na anajivunia kushuhudia wanamitindo wote 
walioshiriki na kuonesha uwezo wao huku akisisitiza kwa zaidi ya miaka 
ishirini amejitolea maisha yake katika sekta ya mitindo, urembo.
Amefafanua
 ameona jinsi mitindo inavyothaminiwa katika nchi za Ulaya na mataifa 
mengine, si tu kama sanaa bali kama alama ya utambulisho, urithi, na 
fahari.Ametoa rai kwa Watanzania kuunga mkono juhudi zinazofanywa na 
wadau pamoja na Serikali chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan katika 
kuinua na kuendeleza sekta ya utamaduni,mitindo na urembo.
Kwa 
upande wake mwanamitindo Elizabeth amesema kukutana kwa mara ya kwanza 
na Millen ilikuwa ni ndoto iliyotimia na amefurahi  kumuona ana kwa ana 
na kwa jinsi alivyo na mafanikio.
“Nimejifuza  kitu kipya kutoka 
kwake, zawadi ambayo alinipa ilikuwa furaha yangu ya pili baada ya kazi 
nzuri ambayo imefanyika, namshuru sana na kumuombea Mungu aendelee 
kumuweka kwa ajili yetu, ni mtu mwema sana, kutoka kwake niliona mtu 
ambaye anataka kuona wanamitindo wengine nchini Tanzania wakifanikiwa.”
Mwanamitindo wa Kimataifa Millen Happiness Magese (kushoto) akimkabidhi hundi ya Sh.milioni tatu Mwanamitindo bora wa Samia Fashion Festival Zanzibar mwaka 2024 Elizabeth Masuka.Hafla ya kukabidhi hundi hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Urban by City Blue iliyopo jijini Dar es Salaam.
 

 
 




 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment