Akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika Uwanja wa Kwamnyani, Mtaa wa Kingugi, Kata ya Kiburugwa, Mbagala, wilayani Temeke leo, tarehe 26 Novemba 2024, Balozi Nchimbi amesisitiza Watanzania kutumia haki yao ya kidemokrasia kuchagua viongozi wenye maono ya maendeleo, amani na utulivu, watakaosimamia vijiji, mitaa na vitongoji kwa miaka mitano ijayo.
Balozi Nchimbi pia amewakumbusha viongozi wa CCM watakaochaguliwa kuwa watumishi wa watu, akisisitiza kwamba Chama hakitasita kuchukua hatua kali dhidi ya viongozi wake watakaotumia madaraka yao vibaya, kwa kuminya haki za wananchi au kuwadhulumu.










No comments:
Post a Comment