Kamati imetoa pongenzi hizo katika Kikao cha Kamati cha kupokea Taarifa ya Urejeshaji wa Mikopo ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Aridhi (KKK) unaotekelezwa katika Halmashauri mbalimbali Nchini kwa Fedha zilizotolewa na Wizara ya Aridhi, kilichofanyika katika Ukumbi wa Anna Makinda Bungeni Jijini Dodoma.
Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela ilipokea mkopo kutoka wizara ya Aridhi jumla ya Shilingi Bil. 3,589,774,000 ambapo ilifanikiwa kurejesha mkopo wote.
Halmashauri nyingine ambazo zimerejesha Mkopo wote ni Halmashauri za Wilaya ya Moshi, Jiji la Mwanza, Wilaya ya Meru, Morogoro Manispaa, Wilaya ya Kilosa, Wilaya ya Geita, Mji wa Bariadi, Wilaya ya Mbozi, Mji wa Tunduma, Wilaya ya Songwe, Wilaya ya Kaliua, Manspaa ya Kigamboni, Mji wa Kibaha Pamoja na Ofisi ya Aridhi ya Mkoa wa Iringa.







No comments:
Post a Comment