Ameyasema hayo leo tarehe 03 Julai, 2024 katika mahojiano maalumu aliyofanya baada ya kutembelea Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji zilizoshiriki maonesho ya Sabasaba.
Ameongeza kuwa Maonesho hayo yamekuwa na mvuto mkubwa kwa kuwa Wizara na Taasisi zilizoshiriki zimeonesha fursa zilizopo katika uwekezaji.
"Tanzania tunaona hii ni fursa nzuri ya kujitangaza kama nchi na kukaribisha wawekezaji mbalimbali kuona fursa za uwekezaji katika nchi yetu" amesema Mhe.Nyongo
Aidha, amepongeza namna ambavyo wafanyabishara wamekuwa wabunifu na makampuni ya nje yaliyokuja kuonesha shughuli za uwekezaji wanazoweza kufanya nchini.


No comments:
Post a Comment