Akizungumza mara baada ya tukio hilo Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mtwara, Mrakibu Oisa Singili amesema askari wa zamu walifika eneo la tukio na kufanikiwa kuudhibiti moto uliokuwa ukiwaka usilete madhara.
Aidha amesema kuwa chanzo cha moto huo kuwaka hakikuweza kufahamika mara moja na uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo halisi cha tukio hilo ambapo asilimia kubwa ya vibanda vya biashara na mali zimeokolewa.





No comments:
Post a Comment