HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 12, 2024

OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAWAPIGA MSASA MAWAKILI WA SERIKALI

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliratibu na kuendeshamafunzo kwa Mawakiliwa Serikali.Mafunzo hayo yalilenga kuwajengea uwezo Mawakili kwenyemasuala mbalimbali yanayohusu sheria ikiwemo Uandishi washeria, mambo muhimu ya kuzingatia kwenye Mikataba naMakubaliano baina ya Nchi au Taasisi, pamoja na mambo yakuzingatia katika kuishauri Serikali kwenye nyanja ya Sheria.

Mafunzo hayo yalifanyika Jijini Dodoma hivi karibuni nakuhudhuriwa na Mawakili takribani mia mbili na tisini (290) kutoka taasisi mbalimbali za Serikali.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi waUmma na Utawala Bora, Mhe George Simbachaweneakizungumza na Mawakili wakati wa ufunguzi wa Mafunzomaalamu kwa Mawakili wa Serikali yaliyoandaliwa na Ofisi yaMwanasheria Mkuu wa Serikali Jijini Dodoma hivi karibuni.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji Dkt. Eliezer MbukiFeleshi akizungumza wakati wa mafunzo kwa Mawakili waSerikali yaliyoandaliwa na kuratibiwa na Ofisi hiyo JijiniDodoma.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Balozi Prof. Kennedy G. Gastorn akifafanua jambo wakati wa Semina naMafunzo kwa Mawakili kutoka Taasisi mbalimbali za Serikaliyaliyofanyika Jijini Dodoma hivi karibuni.
Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Onorius Njole akiwasilishamada kwa washiriki wa mafunzo maalumu kwa Mawakili waSerikali yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu waSerikali Jijini Dodoma hivi karibuni.
Sehemu ya wakufunzi wa mafunzo kwa Mawakili wa Serikaliwakifuatilia kwa ukaribu mada mbalimbali zilizotolewa kwenyemafunzo hayo.
Baadhi ya Mawakili wa Serikali wakisikiliza hoja na madazilizokuwa zikiwasilishwa wakati wa mafunzo kwa Mawakili hao yaliyofanyika jijini Dodoma.
Mawakili wakifuatilia kwa umakini mafunzo yaliyoandaliwa naOfisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali hivi karibuni JjiniDodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe Jaji Dkt. Eliezer MbukiFeleshi akigawa vyeti kwa Mawakili kutoka Taasisi za Serikaliwalioshiriki mafunzo kwa Mawakili yaliyofanyika Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad