HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, June 16, 2024

Doris Mollel akutana na Mkurugenzi wa WHO Geneva

Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Doris Mollel, Bi. Doris Mollel, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Dr. Tedros Adhanom Ghebreyesus, katika Makao Makuu ya Shirika hilo huko Geneva.

Mazungumzo yao yalihusu ushirikiano katika kufikia #AfyaKwaWote na kupunguza vifo vya watoto wachanga barani Afrika na duniani kote.

Katika mazungumzo hayo, Bi. Mollel alielezea jinsi ambavyo Taasisi ya Doris Mollel inafanya kazi nchini Tanzania, hasa katika kuboresha miundombinu ya utoaji huduma kwa watoto wachanga, hasa wale wanaozaliwa kabla ya wakati.

Kwa upande wake, Dr. Tedros aliipongeza Taasisi hiyo kwa juhudi zake katika mapambano hayo na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad