HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, April 24, 2024

WIZARA YA ELIMU YAWATAKA WAZAZI KUTORUHUSU WATOTO KWENDA SHULENI WAKATI WA MVUA KUBWA

NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imewataka wazazi na walezi pindi wanapoona mvua kubwa zinanyesha kutowaruhusu watoto kwenda shule ili kuepuka athari ambazo zinaweza kujitokeza kutoka na mafuriko na kuharibika kwa miundombinu ya barabara katika maeneo mbalimbali nchini.

Wito huo umetolewa leo Aprili 24,2024 jijini Dar es salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizochukuliwa na Wizara baada ya kuharibika kwa miundombinu ya shule.

Amesema  walimu wakuu wanapaswa kuchukua hatua za haraka na kutoa maamuzi pindi wanapoona hali mbaya ya hali ya hewa aidha kwa kuwaruhusu watoto mapema na kufunga shule lakini pia kwa kuwasiliana na wazazi.

Aidha amesema endapo shule zimefungwa kutokana na mafuriko na familia zimehama hivyo kule wanapohamia watoto wanapaswa kupelekwa kwenye shule zilizokaribu ili kuendelea na masomo yao.

"Kama shule zimefungwa na maji yamejaa na familia zimehama kule wanapokwenda wapokelewe wakati maafisa elimu kata wakiwa wanashughulikia taratibu nyingine ikiwa kama mtoto ataendelea kwenye shule hiyo au atakuwepo kwa muda na shule yake ikakarabatiwa anarudi",Amesema.

Prof. Mkenda amesema kuwa Wizara inashirikiana na wazazi ambao watoto wao wanasoma kwenye shule binafsi kuhakikisha wanapata shule ambazo watazichagua wao kwa maelewano yao ili kuwapeleka watoto.

Sambamba na hayo ametoa onyo kwa madereva wa magari ya shule kutopitisha magar hayo kwenye mabwawa ya maji au sehemu yenye maji mengi ili kuepuka kuhatarisha maisha ya wanafunzi.

"Kitu cha kwanza katika shule zetu ni usalama wa watoto wetu na usalama wa wafanyakazi katika taasisi zetu madereva kama wakiona dalili zozote za hatari waache wasije wakaingiza watoto wetu kwenye hatari",

Aidha ameongeza kuwa kamishna wa elimu atoatoa mongozo na kuruhusu mabadiliko katika kalenda ya ufundishaji ili kusaidia kwenye swala la mvua watoto wasiumie. 

Amezipongeza shule binafsi ambazo walipooana hali ya hewa mbaya wakaamua kusitisha kwa muda masomo kwenye shule zao ili kupisha hali hiyo.

Akizungumzia miundombinu iliyoharibika amesema serikali kupitia wizara wamesema wanafuatilia taarifa za hali ya hewa ili waweze kuirejesha miundombinu hiyo ambapo shule ambazo zilizokuwa mabondeni wataangali sehemu salama na kuzijenga.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizochukuliwa na Wizara baada ya kuharibika kwa miundombinu ya shule. Amezungumza leo Aprili 24,2024 katika Ofisi za Wizara jijini Dar es salaam 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizochukuliwa na Wizara baada ya kuharibika kwa miundombinu ya shule. Amezungumza leo Aprili 24,2024 katika Ofisi za Wizara jijini Dar es salaam 





Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua zilizochukuliwa na Wizara baada ya kuharibika kwa miundombinu ya shule. Amezungumza leo Aprili 24,2024 katika Ofisi za Wizara jijini Dar es salaam 

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad