Na Michael Machela

Mshindi wa pili ni timu ya Masti ambayo ilizawadiwa pesa taslimu shilingi laki tano.
Mshindi wa tatu katika mashindano hayo ni timu ya Skylight yenye makazi yake Kijichi Temeke jijini Dar es Salaam ambao walizawadiwa pesa taslimu shilingi laki moja na mshindi wa nne ni Shani Cinema na Morogoro ambao walizawadiwa shilingi elfu hamsini.
Mashindano hayo yalikuwa na mchezaji mmoja mmoja(Singles) ambapo Melkizedeck Amedeus kutoka timu ya Snipers aliibuka kuwa bingwa kwa kumfunga Seif Hamadi 7 – 5 na hivyo kuzawadiwa pesa taslimu shilingi laki tano.
Seif Hamadi alichukuwa nafasi ya pili na hivyo kuzawadiwa shilingi laki mbili.
Mshindi wa tatu mchezaji mmoja mmoja ni Patrick Nyangusi ambaye alizawadiwa shilingi laki moka na mshindi wa nne ni Festo Yohana ambaye alizawadiwa shilingi elfu hamsini.




No comments:
Post a Comment