Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania Mhe. Profesa Makame Mbarawa amesema, ofisi hiyo itapunguza usumbufu kwa wateja wa Bandari ya Dar es salaam kutoka nchini Malawi na watapata huduma zote wakiwa nchini mwao.
Kwa upande wake waziri wa Uchukuzi na ujenzi wa Malawi Mhe. Jacob Hara amesema, ofisi hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa wafanyabiashara wa Malawi na itarahisisha shughuli za usafirishaji wa mizigo kupitia bandari hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mbossa amesema uzinduzi wa ofisi hiyo unatimiza dhamira wa mamlaka hiyo kusogeza huduma zake kwa wateja wake.








No comments:
Post a Comment