HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, December 17, 2023

CHANZO CHA MAJI, MTO RUVUMA KUTUMIKA KUTEKELEZA MRADI WA MAJI CHIPINGO -MKALIWATA

 NAIBU Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amemuagiza  Meneja wa RUWASA wa Wilaya ya Masasi aweze kuhakikisha vijiji nane vya Mnavira, Manyuri, Mkaliwata Chipingo, chikolopola, Mapili, Namyomyo na Raha Leo vinapata huduma ya maji kadri ya usanifu wake.

Mhandisi Mahundi ameyasema hayo  Disemba 16, 2023  Mkoani Mtwara wakati wa ziara yake ambayo ametembelea na kukagua utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa maji wa Chipingo-Mkaliwata wenye thamani ya shilingi Bilioni 3.9

Kadhalika Mhandisi Mahundi ameagiza  vijiji hivyo viweze kufikiwa na huduma ya maji kabla ya mwezi Februari,  2024.

Naye Mbunge wa Jimbo la Lulindi Mheshimiwa Issa Mchungaela ameishukru Serikali kwa  kutekeleza mradi huo, kupitia chanzo cha maji cha Mto Ruvuma

Hata hivyo Mradi wa maji wa Chipingo-Mkaliwata ni miongoni mwa miradi ambayo inatumia chanzo cha maji cha Mto Ruvuma.



 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad