HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, November 7, 2023

Phumzile: Wanaharakati Jikiteni Kuelimisha Watoto wa Kiume

  

Baadhi ya vyeti vya kutambua mchango wa wanaharakati walioisimamisha TGNP Tangu kuanzishwa kwake vilivyotolewa na TGNP katika tamasha 15 jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika Kusini na  Phumzile Mlambo  Ngcuka akizungumza wakati Tamasha la 15 la Sauti ya Pamoja na Miaka 30 ya TGNP lililoambatana na maonesho mbalimbali ya wadau , jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Lilian Lihundi akizungumza  kuhusiana na  Tamasha la 15 la Sauti ya Pamoja na Miaka 30 ya TGNP lililoambatana na maonesho mbalimbali ya wadau , jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi wa TGNP Gemma Akilimali akizungumza kuhusiana na shughuli zilizofanyika na TGNP  kwa miaka 30 wakati Tamasha 15 lililofanyika jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya vyeti vya kutambua mchango wa wanaharakati walioisimamisha TGNP Tangu kuanzishwa kwake vilivyotolewa na TGNP katika tamasha 15 jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya matukio ya picha kwenye Tamasha la  15 la TGNP , jijini Dar es Salaam.



*Akilimali kazi ya Miaka 30 TGNP  ndio inaanza 

Na Chalila Kibuda, Michuzi TV


Makamu wa Rais Mstaafu wa Afrika Kusini na  Phumzile Mlambo  Ngcuka amesema kuwa   wanaharakati wa kifeminia nchini   kujikita  kuelimisha ulinzi wa mtoto wa kiume kwa mustakabali wa haki na usawa wa jinsia.

Hayo ameyabainisha  jijini Dar es Salaam  na Phumzile  kwenye  Tamasha la 15 la  Jinsia pamoja na kuadhimisha  miaka 30 ya kifeminia la Mtandao wa jinsia nchini (TGNP) linalofanyika viwanja vya TGNP jijini Dar e Salaam.


Amesema katika harakati za kukataa ukandamizaji wa aina yoyote  pia suala la ulinzi wa mtoto wa kiume halina budi kuzingatiwa kaa kuendeleza ajenda za kumkomboa kutokana kupitia na changamoto .

"Wanaharakati wa haki za binadamu wasiruhusu aina yoyote ya ukatili  kuanzia kuukataa  mfumo dume kuanzia katika ngazi ya familia na kuongeza kuwa ipo haja ya kuwepo mabadiliko ya kisera na sheria lakini pia jamii kubadilika," amesema Phumzile.

Amesema ipo haja ya kuwa na majukwaa ya wanaume nchini yenye kueleza yanayowahusu lakini pia  yakitumika kuchukua hatua za kupinga ukatili wa kijinsia, wanaopinga ubaguzi  dhidi ya wanawake na  wanaokataa ndoa za utotoni.

Amesema  mfumo dume sio rafiki kwa wanawake na hata wanaume  na  umekuwa  ukiendeleza  ubaguzi hivyo ni muhimu kwa wanaume na watoto wa kiume kuwa miongoni mwa harakati za kuupinga  kwani katika karne hii inahitaji wanaume wenye mshikamano  na wenza wao.

Aidha amesema tamasha la jinsia litumike pia kuwashirikisha wanaume .

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP, Gema Akilimali amesema  licha ya Mtandao huo  kuadhimisha miaka 15 za usawa wa kijinsia lakini  changamoto bado ni nyingi na mshikamano na serikali unahitajika zaidi kwa sasa kuliko huko walikotoka kwa miaka 30 sasa ndio kazi inaanza.

Amesema katika  tamasha hilo la siku nne watatoka na maazimio ya jumla  kwani upo mchango wa TGNP katika harakati mbalimbali ziliifanyika 

Kwa upande  wake Mkurugenzi Mtendaji wa TNGP,  Lilian Liundi amasema  Tamasha la jinsia  ni jukwaa la kuleta sauti kwa pamoja lenye kujadili kwa pamoja na kupanga  mikakati.

"Tamasha hili ni la 15 tangu kuanzishwa  limeweza kuwa na washiriki 2000 hadi 5000 kwa tamasha moja limewafikia watu zaidi ya 35000,"amesema Liundi.

Amesema tamasha hilo limewaleta watu kwa pamoja ukanda wa Afrika na wameendelea kusimama kwenye misingi ya wasisi wao.

Aidha amesema  TGNP imejengwa katika  misingi imara  ya haki na kuondoa mifumo kandamizi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad