Na Mwandishi Wetu.
"Katika Wiki ya maadhimisho ya UWT tunahimizwa kutembelea shule , kwenye madawat ya kijinsia, hivyo ndio maana wao wamegawana katika makundi, kundi moja tumekuja hapa kundi lingine wameenda kwa watoto wa mgongo wazi.
"Kundi la lingnine la UWT limeenda kwa watoto yatima, lingine limeenda shuleni.Kwa hiyo nia na madhubumuni na lengo letu ni kuadhamidha wiki yetu lakini pia kuja kufanya matukio ya kijamii kama tulivyokuja kutembelea hospitali.
" Tumeweza kuona wanawake wenzetu ambao wamejifungua na wana watoto tayari lakini pia tutaenda kuangalia na wodi ya watoto.Hivyo basi tunawashukuru uongozi wa Hospitali kwa moyo wenu wa kukubali sisi kufika hapa."
Aidha wanawake wamekumbushwa kuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukatili wa kijinsia."Mwenyekiti tuna wimbi kubwa la ukatili wa kijinsia linaendelea niwaombe viongozi wote nendeni katika wilaya zenu, kina mama wote nendeni katika wilaya zenu kuhakikisha ukatili wa kijinsia unatokomea nchini kwetu Tanzania.
"Nendeni mahakamani mfungwe vibwebwe mhakikishe mahakimu wanatoa hukumu kwa haki ,watanzania wote ni wamoja tupendane, tusiharibu maisha ya watoto wetu , niwaombe twendeni tukapambane na ukatili wa kijinsia."
Aidha ametumia nafasi hiyo kuelezea jitihada zinazofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo ya wananchi huku akisisitiza Rais anafanya mengi makubwa katika hii nchi yetu.
" Mama halali asubuhi , mchana , jioni tuna muona anapambana kuhakikisha Tanzania inazidi kusonga mbele na kuwa na mafanikio makubwa sana."
No comments:
Post a Comment