HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, October 13, 2023

PROF. NOMBO AVUTIWA NA BIDHAA ZA WANUFAIKA WA SDF

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo amesema amefarijika kuona wanufaika wa Mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi wanafanyia kazi Mafunzo hayo kwa kuzalisha bidhaa mbalimbali kupitia Ujuzi waliojifunza.


Prof. Nombo amesema hayo leo Octoba 13, Kibaha, Pwani alipotembelea banda la Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) katika maonesho ya Maadhimisho ya Juma la Elimu ya Wazima yaliyoanza tangu Octoba 9 na leo ikiwa ndiyo kilele cha maadhimisho hayo.


Akiwa katika banda la TEA, Prof. Nombo alikutana na baadhi ya wanufaika wa Mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi yaliyotolewa kupitia ruzuku ya Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF), ruzuki hiyo ikiwa ni fedha kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na ufadhili wa Benki ya Dunia ambayo hadi mafunzo yanakamilika zaidi ya Watanzania 49,000 walinufaika na mafunzo hayo.


Prof. Nombo amesema, ni jambo la kufurahisha kuwaona wanufaika hao wamethubutu kufanyia kazi kile walichojifunza na kuzalisha bidhaa mbalimbali zikiwa na ubunifu mkubwa ndani yake hivyo, ni wakati muafaka sasa waanze kuzitangaza bidhaa hizo ili kujiongezea wigo mpana wa soko.


‘‘Hizi bidhaa mnazozalisha ni nzuri na nina uhakika zina soko kubwa tuu hapa nchini, anadaeni mikakati ya kuzitangaza ili ziwafikie Watanzania wengi zaidi na mwisho wa siku soko lake lizidi kukua ili muweze kufikia malengo yenu hasa katika ujasiriamali, amesema Prof. Nombo’’


Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), imeshiriki maadhimisho ya Juma la Elimu ya Watu Wazima kupitia Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi ambao unatoa Mafunzo ya Ujuzi kwa lengo la kuwasaidia Watanzania kujihusisha kwenye shughuli za uzalishaji mali ili kujikwamua kiuchumi.

Katika maadhimisho hayo ya kilele cha Juma la Elimu ya Watu Wazima, viongozi mbalimbali walipata fursa ya kutembelea banda la TEA akiwemo Naibu Katibu Mkuu Ofisi Rais TAMISEMI anayehusika na masuala ya Elimu Bw. Charles Msonde na kujionea bidhaa zinazozalishwa na wanufaika wa Mafunzo ya SDF

 









No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad