HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, October 3, 2023

MJUMBE JUMUIYA YA WAZAZI SINGIDA AELEZEA JITIHADA ZA SERIKALI KATIKA KUBORESHA ELIMU

 


MJUMBE wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Singida Ahmed Misanga amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imewekeza  katika kujenga madarasa bora,  kuajiri walimu na kulipia gharama za masomo ili  wanafuzi wapate elimu bora bila ya malipo.

Misanga ameyasema hayo wakati akizungumza katika mahafali ya Shule ya Sekondari Urughu -TAMSIA wilayani Iramba ambapo ametumia nafasi hiyo kueleza namna ambavyo Serikali ya Awamu ya Sita inavyowekeza katika moundombinu ya elimu sambamba na kutoa elimu bure.

"Serikali yetu inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan imewekeza  katika kujenga Madarasa bora,  kuajiri walimu na kulipia gharama za masomo ili  wanafuzi wapate elimu bora bila ya malipo.

Kuhusu wanafunzi wanaojiandaa kufanya mtihani wa Taifa wa kidato cha nne mwishoni mwa Novemba Misanga amewatakia ufaulu  wanafunzi.

Pia amewashauri   walimu na  wazazi kusimamia elimu na malezi bora kwa  wanafunzi ili wapate ufaulu wa juu katika masomo yao na kuwa vijana wenye maadili, tabia nzuri na wenye hofu ya Mungu katika jamii.

Aidha ametumia nafasi hiyo kuwataka  wanafunzi kuwa na nidhamu katika masomo yao kwa kuwa mwanafunzi mwenye nidhamu katika masomo yake, walimu na wazazi siku zote hupata ufaulu wa juu.

Pamoja na hayo amewahimiza walimu na wazazi  kuhakikihasha wanawapa wanafunzi  elimu ya utunzaji mazingira na upandaji miti  kwa vitendo katika maeneo ya shule na kutunza mazingira katika maeneo ya makazi. 

Misanga pia  ametoa zawadi kwa wanafunzi waliopata ufaulu daraja la kwanza na pili pamoja na wanafunzi  wenye nidhamu shuleni  na kugawa vyeti vya uhitimu vilivyoandaliwa na shule. 











 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad