HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, April 28, 2023

JIJI LA TANGA LAMPONGEZA RAIS DKT SAMIA SULUHU KWA KUONYESHA UONGOZI ULIOTUKUKA


Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt Sipora Liana akizungumza wakati wa kikao hicho 

Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shillow akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani la Robo tatu kilichoketi leo kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Mnyema na kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Dkt Sipora Liana.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Hamisi Mkoba akizungumza wakati wa kikao hicho.
Sehemu ya madiwani wakiwa kwenye kikao hicho

Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wakiwa kwenye baraza hilo

Sehemu wa madiwani wakifuatilia hoja mbalimbali



Na Oscar Assenga, Tanga.
HALMASHAURI ya Jiji la Tanga limepongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutimiza miaka miwili madarakani kwa kuonyesha uongozi uliotukuka katika mambo mbalimbali ikiwemo kuendeleza miradi mikubwa iliyoacha na mtangulizi wake hayati Dkt John Magufuli.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mshtahiki Meya wa Jiji la Tanga Abdurhaman Shilloo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani cha Robo ya tatu ambapo alisema licha ya kuendeleza miradi lakini pia ameanzisha mingine mikubwa ikiendana na kupelekea fedha nyingi kwenye ngazi ya Halmashauri ikiwemo Tanga Jiji ambao pia wamenufaina nazo.

Shillow alisema pamoja na hayo lakini Rais Dkt Samia Suluhu amefungua upya milango ya ajira kwa watumishi wa umma baada ya kuingia madarakani kuongeza mishahara kwa watumishi wa umma na kuwapatia unaafuu katika kodi mbalimbali ili waweze kukidhi mahitaji yao na kudumu masiaha yao.

“Lakini jambo jingine ni Rais Dkt Samia Suluhu kuongeza mikopo ya elimu ya juu, kuondosha riba kwa wanafunzi kwenye mikopo hiyo sambamba na kufungua milango ya demokrasia kwa kuenzi utanzania umoja, mshikamano na undugu kwa watanzania bila kujali tofauti za kiitikadi “Alisema Mshtahiki Meya huyo.

Hata hivyo alisema kwamba wanampongeza pia kwakutoa matokeo ya sensa ya watu na makazi iliyofanywa kidigitali kwa mara ya kwanza tokeo nchi ipate uhuru ikiwemo kugawa vishikwambi vilivyotumika katika sensa kwenye idara ya elimu sekondari na msingi za Halmashauri nchini ili kuimarisha elimu na uwekaji wa takwimu za elimu pamoja na kuifungua nchi kwenye mambo ya utalii na mahusiano ya kikanda na kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad