Michezo Inayo wakutanisha wafanyakazi kutoka katika mashirikisho ya Micghezo ya Wafanyakazi wa Wizara, Mikoa, Idara zinazojitegemea na Wakala wa Serikali SHIMIWI), Wafanyakazi wa Mashirika ya Umma na Makampuni Binafisi (SHIMMUTA), Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (SHIMISEMITA) na Wafanyakazi wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama (BAMMATA) maarufu MEI MOSI mwaka huu itafanyika Mjini Morogoro kuanzia tarehe 16 hadi 30 Aprili, 2023 ambako pia kilele cha Sherehe za wafanyakazi KiTaifa zitakakofanyika.
Michezo
itakayoshindaniwa ni Mpira wa Miguu, Netiboli, Riadha, Kuvutana kwa
Kamba, Karata, Bao, “Draft”, Baiskeli na Mpira wa Wavu (Volleyball),
katika Viwanja vya Jamhuri, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA),
Mazimbu, Shule ya Sekondari Morogoro, Kiwanda cha Tumbaku, Magadu na
Chuo cha Ujenzi.
Hadi
sasa Timu zilizo onyesha nia ambazo zipo katika maandalizi ya kushiriki
ni ofisi ya Rais Ikulu, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya
Uchukuzi), Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, wizara ya
Mambo ya nje, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Ofisi ya Taifa ya
Ukaguzi, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro (NCAA), Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya Ulinzi na JKT,
Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Wizara ya Fedha, Wizara ya
Kilimo, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Wizara ya Maliasili na
Benki ya CRDB.
Tunaziomba
timu zinazojiandaa kushiriki zithibitishe kwa maandishi kwa kutaja aina
ya Michezo watakayoshiriki ili kamati iweze kupanga ratiba na kufanya
maandalizi muhimu kama Viwanja na waamuzi kulingana na idadi ya timu.
Aidha,
tunasisitiza timu zote kufika katika kituo cha mashindano (Morogoro)
ifikapo tarehe 14 Aprili, 2023. Timu itakayopangwa katika ratiba endapo
itachelewa kufika na kukuta Mchezo/Michezo yake imepita itahesabika kuwa
amepoteza Mchezo/Michezo hiyo kwa mujibu wa kanuni za mashindano.
Tunawatakia maandalizi mema pia tunawakaribisha Mjini Morogoro.
“Mshikamano Daima”
No comments:
Post a Comment