Na mwandishi wetu
WITO
umetolewa kwa watanzania, hususan wafanyakazi wanaotumia muda mwingi
kufanya kazi wakiwa wamekaa kufanya mazoezi, ili kuimarisha afya zao na
kujiepusha na magonjwa nyemelezi.
Wito huo umetolewa na Mkaguzi
wa Ndani wa Benki ya Biashara ya DCB, Bwana Samwel Mahendela wakati wa
mbio za mwaka huu za Kimataifa za Kilimanjaro Marathon, zilizotimua
vumbi katika mji wa Moshi, Mkoani Kilimanjaro Leo.
Akiongoza
timu ya wafanyakazi 40 wa benki hiyo kushiriki mbio hizo mjini hapa,
Bwana Mahendela alisema, mbio hizi ni muhimu hasa kwa wafanyakazi wa
sekta ya mabenki kwani hutumia muda wao mwingi kuhudumia wateja wakiwa
kwenye viti.
“Kushiriki mbio kama hizi pamoja na mazoezi ya
viungo kwa ujumla vinaimarisha afya ya mwili na akili na kuongeza
ufanisi wa kazi, mara nyingi tunafanya kazi tukiwa tumekaa na pia
hatuna muda wa kutosha wa kufanya mazoezi.
“Natoa wito kwa
wafanyakazi wa sekta za mabenki pamoja na watanzania kuchangamkia mbio
za Kilimanjaro Marathon ili kuimarisha afya zao.
“ Natoa
pongezi pia kwa benki yetu pendwa ya DCB kwa kutuwezesha sisi
wafanyakazi wake kushiriki mbio hizi lakini pia kwa kuisapoti DCB
runners club, DCB tupo Imara tunasonga mbele.
No comments:
Post a Comment