HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, February 15, 2023

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan awaapisha Viongozi Ikulu Jijini Dar es Salaam

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb) kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Balozi Mhe. Pindi Hazara Chana (Mb) kuwa Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 15 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Said Othman Yakub kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Februari, 2023.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb), Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo (Mb) Balozi Mhe. Pindi Hazara Chana pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Said Othman Yakub wakila Kiapo cha Maadili kwa Viongozi kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, 15 Februari, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt. Moses Kusiluka, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa (Mb), Balozi Pindi Hazara Chana, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo (Mb) pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Said Othman Yakub mara baada ya hafla ya Uapisho iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad