Mwenyekiti wa Chama cha Uhifadhi na Uwindaji Tanzania (TACHA,) Kanali Thomas Ndonde (rtd) akizungumza wakati wa mafunzo hayo na kuiomba Serikali kufungua rasmi shughuli za uwindaji zilizozuiwa kwa miaka mitatu sasa, Leo jijini Dar es Salaam.
WAMILIKI na Watumiaji wa silaha za moto za kiraia 
wanaojihusisha na shughuli za uwindaji kupitia Chama cha Uhifadhi na Uwindaji (TACHA) wamepewa mafunzo maalum ya kujengewa uwezo, umahiri na
 kujiamini zaidi katika matumizi ya silaha hizo, huku ombi kubwa likitolewa kwa  Serikali kuruhusu kuendelea kwa shughuli za uwindaji zilizofungwa kwa
 miaka mitatu mfululizo.
Akizungumza
 wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Shabaha leo 
jijini Dar es Salaam Mratibu msaidizi wa mafunzo ya umahiri wa utumiaji 
na utunzaji wa silaha za moto za kiraia nchini  kutoka Shirika la 
Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi (TPFCS,) Ravent Vedasto amesema, 
mafunzo hayo yanatekelezwa kwa mujibu wa sheria ya The Firearms and Ammunition Control 
Act ya mwaka 2015.
"Leo 
tupo katika viwanja hivi vya shabaha chini ya Jeshi la Wananchi Dar es 
Salaam kwa kushirikiana na Chama cha Uhifadhi na Uwindaji  (TACHA,) 
ambao ni wamiliki na watumiaji wa silaha maalum kwa shughuli za 
uwindaji...Tunafanya hivi ili kuwajengea uwezo wa kuzitumia na kubaini 
wale wanaozitumia kimakosa na kuwajengea kujiamini zaidi ili waweze 
kuzitumia vizuri zaidi." Amesema.
Aidha
 amesema, kwa miezi mitatu kuanzia Julai hadi Oktoba mwaka huu jumla ya 
raia 1200 kupitia mwavuli wa TACHA wamesajiliwa na kupatiwa mafunzo na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi Tanzania ( TPFCS.) ambalo pia 
linahusika na utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi, umahiri 
wa matumizi na utunzaji wa silaha pamoja na ulinzi binafsi.
Ameeleza kuwa mafunzo hayo
 pia yanakwenda sambamba na maandalizi na msimu wa Uwindaji ikiwa 
Serikali itaridhia na kuruhusu Uwindaji na Uhifadhi baada ya kutoruhusu 
zoezi hilo kwa miaka mitatu mfululizo.
"Serikali
 yetu ni sikivu na elewa tunaamini itafungua tena anga la uwindaji na 
sisi kama wahusika tuna uelewa kupitia mafunzo mbalimbali ya namna hii 
yanayotolewa na tupo tayari kwa uwindaji kwa kufuata sheria na matakwa 
ya Serikali."
Vilevile 
ametoa wito kwa Wizara ya Utalii na Maliasili kutoa kibali kwa wawindaji
 kwa msimu ujao wa uwindaji ambao kwa kiasi kikubwa huchangia kukua kwa 
uchumi wa Nchi, uhifadhi wa rasilimali za utalii pamoja na kuchangia kwa
 kiasi kikubwa katika utoaji wa ajira.
Chama
 cha Uhifadhi na Uwindaji Tanzania ( TACHA,) kina jukumu la kuwinda na
 kuhifadhi rasilimali za utalii kwa kuzingatia kanuni na miongozo 
iliyowekwa na Serikali na ombi lao kubwa kwa sasa ni kwa Serikali 
kufungua anga la uwindaji lililofungwa kwa miaka mitatu mfululizo.
Mafunzo
 hayo ya siku mbili yameanza kwa nadharia mapema leo na yatahitimishwa 
kwa vitendo ili kuwapika vilivyo wamiliki hao juu ya umiliki na matumizi ya silaha na yamedhaminiwa na kampuni ya Orexy Gas kupitia kampeni ya kutumia nishati ya gesi na kutunza mazingira.
Insp. wa Polisi Vincent Buluba kutoka TPFCS akitoa mada katika mafunzo hayo.
 .jpeg) ASP Hamis Luyeko akitoa mada katika mafunzo hayo ya umiliki wa silaha kwa wanachama wa Uhifadhi na Uwindaji (TACHA,) yaliyolenga kuwajengea umahiri zaidi katika kuzitumia, Leo jijini Dar es Salaam.
ASP Hamis Luyeko akitoa mada katika mafunzo hayo ya umiliki wa silaha kwa wanachama wa Uhifadhi na Uwindaji (TACHA,) yaliyolenga kuwajengea umahiri zaidi katika kuzitumia, Leo jijini Dar es Salaam.

Mafunzo yakiendelea.
 

 
 
.jpeg)



.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)

 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment