HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, November 7, 2022

ROYAL OVEN BAKERY YAWA MWANAFAMILIA WA TotalEnergies TANZANIA

 

KAMPUNI Kinara ya mafuta, TotalEnergies Tanzania imeadhimisha toleo la nne la wiki ya huduma kwa wateja kwa kuingia makubaliano na mgahawa wa Royal Oven ambao umefunguliwa katika kituo cha TotalEnergies Bagamoyo road, Morocco jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo wa wiki ya huduma kwa wateja Mkurugenzi Mkuu wa TotalEnergies Tanzania, Jean Francois Schoepp amesema wateja wao ni kiungo muhimu katika kuendesha, kukuza na kuendeleza biashara pamoja na kukidhi mahitaji ya wateja wao.

Amesema, wiki ya huduma kwa wateja kwa mwaka 2022 imebeba kauli mbiu ya 'Pamoja Kila Hatua ' huku msisitizo ukiwa si kwa huduma ya mafuta pekee bali huduma nyinginezo ikiwemo bidhaa za  vilainishi, huduma za kuosha magari, maduka ya Bonjour na huduma kutoka Royal Oven Bakery.

Ameeleza kuwa, Kampuni hiyo imekuwa ikiweka kipaumbele kwa wateja wao katika kuhakikisha wanakidhi mahitaji yao kupitia huduma zinazotolewa na TotalEnergies.

"Katika wiki hii ya huduma kwa wateja Afrika, hapa Tanzania tunawakaribisha wateja wetu kutembelea vituo vyetu kote nchini na kufurahia huduma zinazotolewa na TotalEnergies na kufurahia ofa zinazotolewa pamoja na kupokea maoni yenu yatakayoboresha huduma zetu zaidi." Amesema.

Katika wiki hiyo ya huduma kwa wateja watakaopata huduma katika kituo cha TotalEnergies Bagamoyo road watapata ofa ya kujipatia beef burger moja bure wakununua bidhaa ya beef burger katika mgahawa Royal Oven.

Aidha amesema kuwa TotalEnergies inaamini kuwa wiki ya huduma kwa wateja ni zaidi ya kuisherehekea bali ni muhimu katika kupokea na kubadilishana maoni na kuwahimiza wateja wao kutumia kurasa za mitandao ya kijamii ya kampuni hiyo kutoa maoni yao ambayo yatafanyiwa kazi na kuboresha zaidi huduma zitakazokidhi matarajio za wateja wao.

Pia ameupongeza mgawaha wa Royal Oven Bakery kwa kuichagua TotalEnergies na kushirikiana nao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Royal Oven Bakery Patrick Meme amesema wamekuwa sehemu ya TotalEnergies kwa kufungua tawi katika kituo cha Bagamoyo road, Morocco na wateja watapata huduma bora za bakery kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa nne usiku.

"Tunawaalika wateja wetu kuja kufurahia wiki ya huduma kwa wateja pamoja na kampuni kinara ya TotalEnergies hapa Bagamoyo road Morocco na kupata ofa katika mgahawa pendwa wa Royal Oven." Amesema.
Mkurugenzi Mkuu wa TotalEnergies Tanzania Jean Francois Schoepp akitoa huduma kwa mmoja wa wateja waliofika kituoni hapo kupata huduma.
Mkurugenzi Mkuu wa TotalEnergies Tanzania Jean Francois Schoepp akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi na TotalEnergies na Royal Oven Bakery.

Muonekano wa Royal Oven Bakery katika kituo cha TotalEnergies Bagamoyo road, Morocco.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad