Kampuni ya simu ya Halotel na wafanyakazi wake leo wameshiriki katika 
zoezi la kuchangia damu ikiwa ni sehemu ya kusheherekea na kuadhimisha 
miaka 7 ya kampuni na utoaji wa huduma za mawasiliano.
Zoezi la 
kuchangia damu ni majawapo ya taratibu ambazo Kampuni hiyo imejiwekea 
kama msaada wa kurudisha shukrani kwa jamii pamoja na kuunga mkono 
jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya katika kukabiliana na 
changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au vituo vya kutolea huduma
 za afya.
Akizungumza wakati wa zoezi hilo katika ofisi za makao 
makuu ya Halotel, Mkuu wa kitengo cha Bidhaa na Mawasiliano Halotel, Bi.
 Sakina Makabu amesema kuwa katika kuhakikisha tunasaidia sekta hii ya 
afya nchini, tumeona ni vyema kuchangia damu ili kuokoa maisha ya 
watanzania wenye uhitaji hasa wa damu kwenye hospitali mbalimbali 
nchini.
“Takwimu kupitia wizara ya afya nchini zinaonesha kwamba,
 uhitaji wa damu ni mkubwa sana kwa kuwa damu inahitajika sana na mama 
wajawazito, watoto, watu waliopata ajali pamoja na wanaofanyiwa 
upasuaji", hivyo sisi kama Halotel kwa kushirikiana na Taasisi ya Tiba 
ya Mifupa Muhimbili (MOI) tumeendeleza zoezi hili la kushiriki na 
kuchangia damu kama hitaji maalum na ishara ya upendo kwa vitendo kwa 
watanzania ambao pia ndio wateja wetu”. Alisema Sakina.
“Tunatambua
 changamoto mbalimbali zinazoikumba sekta ya afya hasa katika upande wa 
uhitaji na upatikanaji wa damu katika hospitali na vituo vya afya kwa 
wagonjwa na kuamua kuendelea kuunga mkono juhudi za utatuzi wa 
changamoto hii kwa kujali na kutambua umuhimu kama kampuni na 
wafanyakazi tumeamua kurudisha upendo huu kwa jamii. Aliongeza Sakina”
Akiongea
 wakati wa zoezi hilo la uchangiaji damu mmoja kati ya wafanyakazi 
waliochangia damu Bw;Dalili Musa alisema, “Tunajisikia furaha sana 
kushiriki katika zoezi hili moja kwa moja kwasababu huduma hii 
tuliyoifanya hapa kinaweza kuonekana ni kidogo ila kinaenda kuokoa 
maisha ya watu na hakika ni kitendo cha kuonesha upendo na kinaleta 
faraja Sana.
Kwa upande wa Uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa, 
Daktari wa dawa za usingizi katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili 
(MOI), Bw; Juma Said Kabelele alisema “ Tumefarijika sana kwa kuja hapa 
na kufanya zoezi hili la kutoa damu na kampuni ya Mawasiliano ya Halotel
 na wafanyakazi wake, tunawashukuru sana kwa kuthamini afya za wananchi 
lakini pia kwa kuunga mkono jitihada za kuisaidia sekta ya afya nchini. 
Hii ni hatua kubwa na endelevu kwetu sisi katika kuimarisha ushirikiano 
wetu na Halotel kwa kiwango cha juu hasa katika kuboresha sekta ya afya 
kwa ujumla”.
“Tunapenda kutoa rai kwa watu binafsi, makampuni na 
Taasisi mbalimbali kuweza kujitoa na kushiriki zaidi katika zoezi la 
uchangiaji damu popote walipo nchini ili kuendelea kuipa ushirikiano 
sekta ya afya nchini katika kukabiliana na tatizo la upungufu wa damu 
katika benki ya taifa ya damu na hospitali mbalimbali maan mahitaji ni 
makubwa sana na kila iku kuna idai kubwa ya wagonjwa wanaohitaji huduma 
ya kuongezewa damu kulingana na tatizo husika la afya, hivyo utaweza 
kuokoa Maisha ya watanzania wengi kwa Pamoja.” Aliongeza Mvungi.
Licha
 ya kampuni ya simu ya Halotel kupiga hatua kubwa katika kusambaza 
huduma za mawasiliano na intaneti yenye kasi na ubora wa hali ya juu ya 
4G maeneo mengi nchini, kampuni hii imekuwa ikijihusisha na kutoa 
misaada mbalimbali kwa jamii ya watanzania. Hii ni katika kuonesha jinsi
 inavyothamini na kujali jamii ya watanzania kwa nyanja mbalimbali, 
ikiwemo kuboresha sekta ya afya na zinginezo kama moja ya kipaumbele cha
 kampuni ya hii kwa maendeleo ya watanzania na nchi kwa ujumla.Meneja
 wa huduma za Kidigitali Halotel Caroline Majaliwa akishiriki katika 
zoezi la uchangiaji damu lililoendeshwa na Kampuni ya simu ya Halotel 
pamoja na Wafanyakazi kwa kushirikiana na Taasisi ya Tiba ya Mifupa 
Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja ya msaada wa kurudisha shukrani kwa jamii 
katika kuelekea kilele cha kuadhimisha na kusherehekea miaka saba (07) 
ya kutoa Huduma za mawasiliano hapana nchini pamoja na kuunga mkono 
jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya katika kukabiliana na 
changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au vituo vya kutolea huduma
 za afya.
Baadhi
 ya Wafanyakazi wa Kampuni ya Simu ya Halotel Bw: Dalili Musa Mkuu wa 
kitengo cha Usimamizi wa Mawasiliano ya Simu (wa kwanza Kushoto) na Bw; 
Pius Joseph Tibasiga Afisa Manunuzi Halotel ( Wa pili kushoto) 
wakishiriki katika zoezi la uchangiaji damu lililoendeshwa na Kampuni ya
 simu ya Halotel pamoja na Wafanyakazi kwa kushirikiana na Taasisi ya 
Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja ya msaada wa kurudisha 
shukrani kwa jamii katika kuelekea kilele cha kuadhimisha na 
kusherehekea miaka saba (07) ya kutoa Huduma za mawasiliano hapana 
nchini pamoja na kuunga mkono jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya
 katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au 
vituo vya kutolea huduma za afya.
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma na Mawasiliano Halotel Sakina Makabu 
akiongea na waandishi wa Habari leo katika Ofisi za makao Makuu Halotel 
wakati wa zoezi la uchangiaji damu lililoendeshwa na Kampuni ya simu ya 
Halotel pamoja na Wafanyakazi kwa kushirikiana na Taasisi ya Tiba ya 
Mifupa Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja ya msaada wa kurudisha shukrani kwa
 jamii katika kuelekea kilele cha kuadhimisha na kusherehekea miaka saba
 (07) ya kutoa Huduma za mawasiliano hapana nchini pamoja na kuunga 
mkono jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya katika kukabiliana na 
changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au vituo vya kutolea huduma
 za afya.
Daktari
  wa dawa za usingizi katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), 
Bw; Juma Said Kabelele  akiongea na waandishi wa Habari leo katika Ofisi
 za makao Makuu Halotel wakati wa zoezi la uchangiaji damu 
lililoendeshwa na Kampuni ya simu ya Halotel pamoja na Wafanyakazi kwa 
kushirikiana na Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja 
ya msaada wa kurudisha shukrani kwa jamii katika kuelekea kilele cha 
kuadhimisha na kusherehekea miaka saba (07) ya kutoa Huduma za 
mawasiliano hapana nchini pamoja na kuunga mkono jitihada za serikali 
kupitia Sekta ya Afya katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa damu 
katika hospitali au vituo vya kutolea huduma za afya.
 Afisa Masoko Kitengo Halopesa Roxana Christopher Kadio akishiriki 
katika zoezi la uchangiaji damu lililoendeshwa na Kampuni ya simu ya 
Halotel pamoja na Wafanyakazi kwa kushirikiana na Taasisi ya Tiba ya 
Mifupa Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja ya msaada wa kurudisha shukrani kwa
 jamii katika kuelekea kilele cha kuadhimisha na kusherehekea miaka saba
 (07) ya kutoa Huduma za mawasiliano hapana nchini pamoja na kuunga 
mkono jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya katika kukabiliana na 
changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au vituo vya kutolea huduma
 za afya.
 Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu Halotel Bw: Thang Bui Van akiwa 
katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo katika 
ofisi za Makao Makuu ya Halotel leo katika zoezi la uchangiaji damu 
lililoendeshwa na Kampuni hiyo pamoja na Wafanyakazi kwa kushirikiana na
 Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ikiwa ni moja ya msaada wa 
kurudisha shukrani kwa jamii katika kuelekea kilele cha kuadhimisha na 
kusherehekea miaka saba (07) ya kutoa Huduma za mawasiliano hapana 
nchini pamoja na kuunga mkono jitihada za serikali kupitia Sekta ya Afya
 katika kukabiliana na changamoto ya uhaba wa damu katika hospitali au 
vituo vya kutolea huduma za afya.
 
 
 
Friday, October 7, 2022
Halotel yasherehekea miaka 7 ya utoaji huduma za Mawasiliano kwa kuchangia damu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment