Kampuni
ya uuzaji na unganishaji wa magari na mitambo ya Gf Trucks &
Equipment’s Ltd imeibuka kuwa kampuni ya kwanza inayouza na kusambaza
Magari na mitambo ukanda wa mikoa ya kanda ya ziwa.
Hayo
yamejiidhihirisha wakati wa kufunga maonesho ya 5 ya teknolojia ya
madini mkoani Geita na kuibuka kampuni bora ya usambazaji na uuzaji wa
mitambo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo na
Waziri wa Viwanda na uwekezaji Ashatu Kijaji,Afisa masoko na mauzo wa
kampuni ya GF Poul Msuku alisema wanafurahia kuibuka washindi katika
kipengele hicho na wanachukua tuzo hiyo kama chachu ya kujipanga na
kuongeza nguvu kaitia uwekezaji kwa kanda ya ziwa.
Gf Trucks
ambao ni wauzaji wa mitambo na mashine za migodini aina ya XCMG, na
magari ya kubebea mizigo ya FAW na Hongyang wana wateja wengi
wanaojihusisha na Uchimbaji wa madini na shughuli za usafirishaji
nchini,
Pia Gf waliitumia siku ya kufunga maonesho kwa kukabidhi
Mtambo wa kuchimbia madini kwa mteja aliyenunua katika maonesho hayo ya
madini kwa bei ya punguzo.
Pia Waziri Kijaji aliwataka Gf
kuwekeza zaidi katika kwawezesha wachimbaji wadogowadogo ili waweze
kujikomboa na kwa kuwawekea utaratibu rahisi kumudu gharama, ikiwemo
mikopo rahisi na pia aliwataka wachimbaji hao kuchapa kazi itakayoweza
kumwongezea kipato na kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi.
Nae
Mkuurugenzi wa kampuni ya G Unity Squre Ltd,Ezekiel Rembo aliwashukuru
GF kwani kwa kushiriki katika maonesho hayo, wameweza kununua mashine
hiyo (XCMG) kwa gharama nafuu tofauti kama wangeifuata Dar essalaam na
kwamba ameokoa zaidi ya shilling million 10 ikiwamo gharama ya mafuta
kuitoa Dar hadi Geita alimaliza .
Waziri wa Viwanda na uwekezaji, Ashatu Kijaji akimkabidhi Tuzo ya mshindi wa kwanza kwa makampuni yanayouza na kusambaza Magari na mitambo Migodini Afisa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Gf Trucks & Equipments Ltd ,Poul Msuku wakati wa kufunga maonesho ya Madini mkoani Geita.
Waziri wa viwanda na uwekezaji Ashatu Kijaji akimkabidhi funguo ya mtambo wa kuchimbia Madini (Excavator ) ya XCMG Mkurugenzi wa kampuni ya G Unity ,Ezekiel Rembo baada ya kununua katika maonyesho ya madini kwa punguzo malum mkoani Geita
Mkurugenzi wa E Unity akiangalia mtambo wa Excavator baada ya kukabidhiwa katika viwanja vya maonyesho
No comments:
Post a Comment