-Hatua hiyo ni sehemu ya kusherekea miaka 90 ya kampuni hiyo kubwa duniani
Kampuni
Eureka Trading Tanzania imezindua bidhaa tano mpya za wine, hatua
ambayo inaipa nguvu zaidi kampuni hiyo yenye miaka 90 kwenye soko la
dunia.
Eureka Trading ni sehemu ya kampuni mama ya Oxenham yenye
makao yake nchini Mauritius ambayo ilianzishwa mwaka 1932 ikitambulika
kwa bidhaa zenye viwango vya kimataifa.
Akizungumza wakati wa
uzinduzi wa bidhaa hizo, Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Alan Oxenham
alisema kwa kutumia uzoefu wa kampuni hiyo nchini Mauritius,
wamejizatiti kutumia ubora huo kuleta ladha tofauti kwenye soko la
Tanzania.
“Nina furaha kuwa sehemu ya familia hii kubwa na
kutambulisha bidhaa hizi kwa jina la Eureka Trading Tanzania, bidhaa
zetu hizi zimefanikiwa kwa kiwango kikubwa nchini Mauritius na
tunafuraha kuzileta hapa nchini,” alisema.
Bidhaa hizo ni
Frizante grape fruit, Frizante lime, Oxano semi sweet, Avino sweet red
18% vol and Oxenham old port zenye sifa tofauti tofauti kulingana na
mahitaji ya mteja ikiwamo ladha pamoja na kiasi cha kilevi.
“Bidhaa yetu ya Frizante Grape Fruit ni laini na yenye ladha ya rose na
yenye harufu nzuri sana.Ni kinywaji kizuri kwa kunywa kabla ya kula
lakini pia kinafaa kwa matumizi mengine.Ni kinywaji mahususi kwaajili ya
msimu wa joto ili kukufanya kujisikia murua,” alisema.
Frizante
lime ni kinywaji chenye povu (bubble) na chenye harufu nzuri na yenye
kuvutia.Ni kinywaji kinachofaa kwa matumizi ya aina zote na wakati
wowote.
Kuhusu Oxano Semi Sweet, Alan Oxenham anasema “Kina
rangi nzuri ya dhahabu na chenye harufu nzuri sana.Kimetengenezwa kwa
viungo vyenye ladha ya matunda na mimea.”
Avion Sweet red 18%
ni kinywaji chenye ladha tamu na muonekano wa thamani na harufu nzuri
wakati Oxenham Old Port imetengenezwa maalumu kwaajili ya kuupa mwili
joto wakati wa baridi.
Bidhaa hizi kwa sasa zinapatikana jijini Dar es Salaam lakini zitasambazwa kwenye Mikoa mingine siku za hivi karibuni.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Alan Oxenham akizungumza wakati wa uzinduzi wa bidhaa za Eureka Tanzania.
No comments:
Post a Comment