*Zimo za utitiri wa kodi, mateso kwa wavuvi wanaovua Ziwa Victoria
*Wataja hatua kwa hatua yanayosababisha sekta ya uvuvi kudorora
Na Mwandishi Wetu, Mwanza
MAKAMU
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Kanali Mstaafu
Abdulrahman Kinana amepokea malalamiko 13 ya wavuvi wa samaki katika
Ziwa Victoria ikiwemo utitiri wa kodi pamoja na mateso wanayoyapata
wavuvi wanapokuwa ziwani ambapo yote hayo ameahidi kuyafikisha katika
mamkala husika kwa ufumbuzi.
Aidha
amesema Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kutatua changamoto
mbalimbali zikiwemo za kisheria, hivyo changamoto zilizotolewa na wavuvi
zitafanyiwa kazi kwa ajili ya kuifanya sekta ya uvuvi kuwa na tija
zaidi.
Kinana
ameyasema hayo leo jijini Mwanza alipozungumza na wavuvi wa Kanda ya
Ziwa Victoria katika ukumbi wa BoT, akiwa katika ziara ya kukagua uhai
wa Chama na utekelezaji wa Ialani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025.
“Ndugu
zangu nimekuja hapa kuwasikiliza kwa sababu mbili, kwanza Serikali hii
ni ya Chama Cha Mapinduzi na pili nimekuja kuwasikiiliza, nimewasikiliza
vizuri na kwa umakini, nimesikiliza risala pamoja na wasemaji wengine
na yote yaliyozungumzwa na mliyosema tumeandika.
“Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lengo lake kuu ni kuwasaidia
Watanzania ili kipato chao kiendelee kuongezeka wanapofanya bisahara.
Tunapozungumzia sekta binafsi imara nyingi tunawafikiria wawekezaji
wakubwa wa viwanda na wakati mwingine tunawafikiria hata watu kutoka nje
pekee.
“Ieleweke
ukiifikiria sekta binafsi ni hawa (wajasiriamali wadogo) na ndio wenye
viwanda vidogo, wanajituma ili wawe na maisha bora. Serikali haiwezi
kumwondolea mtu umasikini wake, lakini inaweza kutengeneza mazingira
mazuri, sheria na kanuni nzuri ili iwe rahisi kwa mtu kufanya shughuli
zake kwa ufanisi na kwa faida, hiyo ndio kazi ya Serikali,” alisema
Kinana.
Aliongeza
kuwa, wakati anasikiliza risala ya wavuvi miongoni mwa malalamiko ni
uwepo wa kodi 11 ambazo ili uweze kumudu lazima uwe na kipato kikubwa
huku akieleza kushangwa na uwepo wa kodi ya maegesho vyombo vya uvuvi.
“Imenifanya
nicheke eti kuna kodi ya ‘parking’ yaani kodi zote wamechukua mwisho wa
siku wamekuja na parking. Sasa hivi kodi nyingi kidogo, natolea mfano
tu., lakini niwaambie nia ya Rais na nimemsikia Rais amezungumza juu ya
malengo manne aliyonayo maana la kwanza ni kuleta maridhiano kwa
Watanzania, kuleta maboresho ya serikali katika muundo, sheria, sera na
kanuni ili maisha ya watu yawe bora zaidi.
“Sasa
katika kuboresha mambo risala yenu hii itatizamwa namna gani tunaweza
kubadili mambo yao yawe bora zaidi. Risala yenu itatazamwa namna gani
tunaweza kubadilisha mambo ambayo yapo kama 14,” alisema.
Aidha,
alisema baada ya miaka mingi Rais Samia ametoa fedha za ruzuku kwa
ajili ya wakulima, lakini ametoa fedha za ruzuku kwa baadhi ya wavuvi
ambapo ametoa fedha kwa ajili ya kutengeneza viamba na kwa mkoa wa
Mwanza umepata viamba 42.
“Kwa
hiyo Rais ana lengo nzuri , hawezi Rais anaweza kuwa na nia njema ,
malengo mazuri lakini watanzania lazima tumsaidie ili kazi na malengo
yaweze kufikiwa. Risala yenu hii ni moja ya njia ya kumsaidia Rais Samia
kuwasaidia Watanzania kuondokana na umasikini vile vile kuwa matajiri
kupitia uvuvi,”alisema Kinana.
Hivyo
amewaahidi kupitia nafasi aliyonayo vikao alivyonavyo , kwa namna
anachohusika na Chama chake na Serikali yake hayo mambo yote
waliyoyasema yatashughulikiwa ipasavyo.
“Sina
jibu la kutoa hapa na si vizuri nikaanza kuyajibu haya mambo kwasababu
mliniita niwasilikize , nimewasiliza mmeniomba na kunitaka kama Chama
kinachounda Serikali yake kitafute namna ya kutatua matatizo haya.
“Niwaahidi
nitakwenda kuwahakikisha haya masuala yote yaliyotolewa humu ndani
yanapata majibu na yanapata ufumbuzi .Yako yanahusu Serikali ya
utekelezaji, Wizara , sera, sheria pamoja na kanuni zinazotungwa na
Serikali hasa Wizara .Nitatizama namna gani nitasaidia ili na ninyi kwa
yale mliyoyasema yaweze kufanikiwa,”alisema Kinana.
Awali
akisoma risala ya wavuvi, Katibu wa Kamati ya Ushauri wa Wavuvi Ziwa
Victoria Mayalu Kasiri, alielezea changamoto na matatizo yanayosumbua
sekta ya uvuvi na kusababisha kudorora.
Ametaja
changamoto hizo ni kukithiri kwa uvuvi haramu ambalo limekuwa likiitesa
sekta hiyo katika Ziwa Victoria, pili biashara holela ya mabondo ya
Sangara ambayo inachangia iwepo wa uvuvi haramu , uvamazi, utekeji na
unyang’anyi wa samaki kwa wavuvi ziwani.
Changamoto
nyingine ni muundo wa Wizara ya Uvuvi ambapo ameeleza sio mzuri kwa
kuwa ina mkurugenzi mmoja ambaye ndiye anayeratibu shughuli zote za
Wizara wakati yupo makao makuu ya Wizara.
“Tunaomba
Serikali kuweka mfumo rasmi wa wavuvi kwani kumekuwa na matatizo mengi
ya wavuvi kuhusu kukosa mitaji na zana bora za uvuvi, hivyo tunaomba
Serikali yetu kuweka mfuko maalumu kwa ajili ya wavuvi tu kuliko ilivyo
sasa kupitia benki ya kilimo ambayo mvuvi akienda hakopeshiki mpaka
alete dhamana ya mali zao kama hati ya nyumba,”amesema.
Ametaja
changamoto nyingine tozo ya ushuru wa wavuvi ambazo ziko 11 na ambapo
meeleza kwa muda mrefu sasa wamekuwa na utitiri wa tozo na ushuru ambazo
hulipwa na wavuvi na kufanya wabebe mzigo mzito na hatimaye washindwe
kujikwamua dhidi ya umasikini.
Wakati
changamoto nyingine ni ulinzi na usalama wa mali za wavuvi kwani kwa
muda mrefu sasa wamekuwa wakipatwa na majanga pindi wawapo katika kazi
zaa ziwani.Changamoto nyingine ni mafuta kwa ajili ya wavuvi ambayo
alisema wamekuwa wakitumia nishati ya mafuta ya petrol, dizeli na mafuta
ya taa ambayo bei yake kwa sasa iko juu.
Kasiri
ametaja changamoto nyingine ni sheria za uvuvi na kanuni zake zilizopo
sasa ni kandamizi kwa wavuvi kwani hazitoi mwanya wa mvuvi kupata haki
zake kama raia wa Tanzania. Wakati nyingine ni bei kubwa ya zana za
uvuvi.
Changamoto
ya 10 ni mazalia ya samaki katika ziwa victoria kwani sehemu nyingi
yanaharibiwa ,changamoto nyingine ni matumizi mabaya ya taa za sola
ziwani ambapo kuna baadhi ya wavuvi huzibadilisha na kuzitumbukiza
ziwani kuweka taa mbili kwenye Sikimai mojana zaidi ya Wati 10, kutumia
betri kubwa ya uwezo wa taa na kutumia ambazo hazijafanyiwa utafiti.
Akiendelea
kutaja changamoto hizo alisema iko pia fidia kwa wavuvi walioathiriwa
na operesheni sangara mwaka 2018 na changamoto ya mwisho ni kutokuwepo
na bodi ya uvivi ambapo wameomba iundwe ili kuratibu masuala ya uvuvi
kwa ukaribu zaidi.
Makamu
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman
Kinana, akizungumza na wavuvi na wadau wa Uvuvi Kanda ya Ziwa, katika
ukumbi wa BoT, leo Septemba 5,2022 jijini Mwanza, akiwa katika hitimisho
ya ziara yake kukagua uhai wa Chama na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi
ya CCM 2020-2025. (Picha zote na Fahad Siraji wa CCM).
Makamu
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kanali Mstaafu Abdulrahman
Kinana, akizungumza na wavuvi na wadau wa Uvuvi Kanda ya Ziwa (hawapo
pichani), katika ukumbi wa BoT, jijini Mwanza leo Septemba 5, akiwa
katika hitimisho ya ziara yake ya kukagua uhai wa Chama na utekelezaji
wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025
No comments:
Post a Comment