-Wateja wanaoufungua akaunti za amana kupata riba hadi asilimia 11 papo hapo
BancABC
Tanzania ambayo ni kampuni tanzu ya Atlas Mara na ambao imeorodhesha
kwenye soko la hisa la London, imepiga hatua nyingine kwenye soko baada
ya kuzindua kampeini maalum inayolenga kuwanufaisha wateja wanaofungua
akaunti za amana.
Kwenye
kampeini hiyo ambayo inaanza leo na kuendelea mpaka Disemba 15 mwaka
huu, wateja wa BancABC Tanzania watakaofungua akaunti za amana watapata
riba ya hadi asilimia 11 papo hapo.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam wakati wa kuzindua kampeini hiyo, Afisa Mkuu
Muendeshaji BancABC Tanzania Joyce Malai alisema kuwa benki hiyo
imezindua kampeini ambapo wateja wanaofungua akaunti za amana watapata
riba ya asilimia 11 kuanzia leo mpaka katikati ya mwezi Disemba mwaka
huu. Riba hiyo italipwa papo hapo huku salio ya akaunti ikiendelea
kubaki salama mpaka muda wa ukomavu atakapofika.
‘Hii
ni moja ya ofa bora kabisa kwenye soko na naomba kutumia hii fursa
kuwaomba wateja wetu na Watanzania ambao hawana akaunti na sisi kutumia
nafasi ili kufaidika na kampeini hii’, unavuna kabla ya kupanda, alisema
Malai.
Malai
alisema kuwa BancABC imejidhatiti kufikia mahitaji ya wateja na
kuhakikisha kwamba wanakua pamoja na benki hiyo. “Tunathamini jinsi
wateja wetu wanavyotuunga mkono na hiyo ndio sababu sisi kama benki
tumeamua kuwazawadia ofa hii kabambe’.
Aliongeza
kuwa BancABC ipo tayari kukubali wateja kufungua akaunti za amana kwa
kipindi cha robo ya mwaka, nusu au mwaka na riba italipwa papo hapo kwa
akaunti zote hizo. ‘Sisi kwetu mteja ni mfalme na ndio sababu tuko
tayari kusikiliza’, Malai alisema.
Kwa
upande wake, Meneja wa Kitengo wa Wateja wa Rejareja na Biashara
Lillian Mwakitalima alisema kuwa kinachotakiwa kufanywa na mteja yeyote
ili aweze kujipatia ofa hii nikufika kwenye matawi yetu nchini kote na
kufungua akaunti ya amana ya muda maalumu ambapo riba hiyo italipwa papo
hapo, lengo ni kukupa uhuru wa wa kupanga kwa sasa au kwa baadae.
‘Mteja
anapaswa kutembelea tawi lolote la BancABC Tanzania na kufungua akaunti
ya amana na riba yake kulipwa hapo hapo, na mteja anaweza kutumia riba
kwa kufanya manunuzi, kufanya matembezi au kuwanunulia zawadi
wanafamilia au marafiki’, Mwakitalima aliongeza.
‘Mteja
pia anaweza kutumia akaunti hii ya amana kupata mkopo. Tunakaribisha
wateja watutembelee kwani sisi tuko huru kuwasikiliza’, alisema
Mwakitalima huku akiongeza kuwa mteja anaweza kuwasiliana nasi kwa
kupiga 0779 111000 au kutembelea moja ya matawi yetu waliopo Dar es
Salaam, Dodoma, Mwanza na Arusha kasha kufungua akaunti ya amana na
kuanza kufaidika mara moja.
Meneja
wa Kitengo wa Wateja wa Rejareja na Biashara BancABC Tanzania Lillian
Mwakitalima (kushoto) akizungumza jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
baada ya kuzindua kampeini maalum inayolenga kuwanufaisha wateja
wanaofungua akaunti za amana ambapo kwenye kampeini hiyo ambayo inaanza
leo na kuendelea mpaka Disemba 15 mwaka huu, wateja wa BancABC Tanzania
watakaofungua akaunti za amana watapata riba ya hadi asilimia 11 papo
hapo. Kulia ni Afisa Mkuu Muendeshaji BancABC Tanzania Joyce Malai.Meneja
wa Kitengo wa Wateja wa Rejareja na Biashara BancABC Lillian
Mwakitalima (kushoto) akiwa na Afisa Mkuu Muendeshaji BancABC Tanzania
Joyce Malai (kulia) wakionyesha bango mara baada ya kuzindua kampeini
maalum inayolenga kuwanufaisha wateja wanaofungua akaunti za amana
ambapo kwenye kampeini hiyo ambayo inaanza leo na kuendelea mpaka
Disemba 15 mwaka huu, wateja wa BancABC Tanzania watakaofungua akaunti
za amana watapata riba ya hadi asilimia 11 papo hapo.
No comments:
Post a Comment