HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Friday, August 19, 2022

NSSF yaweka rekodi nyingine ya mafanikio katika ukuaji wa Mfuko

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya utendaji wa Mfuko pamoja na vipaumbele vya Mfuko kwa mwaka wa fedha 2022/23.

Baadhi ya wafanyakazi wa NSSF na waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba leo Agosti 19, 2022 jijini Dar es Salaam wakati akiwasili utekelezaji wa  Bajeti ya 2022/2023.

*Mkurugenzi Mkuu asema mafanikio hayo yamechangiwa sana katika Serikali ya awamu ya sita

Na Mwandishi wetu
KURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Masha Mshomba, amesema Mfuko umepata mafanikio makubwa na umekua kwa kasi.

Mshomba ameyasema hayo leo Agosti 19,2022 jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa ya Utendaji wa Mfuko pamoja na Vipaumbele vya Mfuko kwa mwaka wa Fedha 2022/23.

"Tumepata mafanikio makubwa katika suala zima la ukuaji wa Mfuko na hii imesababishwa na sababu kadhaa ikiwemo kuweka misingi imara na madhubuti ya ukusanyaji wa mapato," alisema.

Mshomba amesema ukuaji huo ni mkubwa tofauti na miaka miwili ya nyuma iliyopita ambapo thamani ya Mfuko ilikuwa ni Shilingi Trilioni 4.3 na kuwa ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la makusanyo ya michango.

Amesema katika mwaka wa fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022, Mfuko ulikusanya zaidi ya Shilingi Trilioni 1.42 kwamba makusanyo hayo ni zaidi ya hata bajeti ambayo walijipangia iliyokuwa Shilingi Trilioni 1.38.

Mshomba amesema pia Mfuko umeboreshaji sana udhibiti wa matumizi jambo ambalo limechangia ukuaji wa NSSF.

Mafanikio mengine yaliyopatikana, amesema ni uboreshaji wa huduma hasa kwa kutumia mifumo mbalimai ya TEHAMA ambapo sasa mwanachama na wadau wanaweza kupata huduma popote walipo bila ya kufika katika ofisi za NSSF kwa kutumia mifumo ya waajiri na wanachama yaani Employer Potal na Member Potal.

Mshomba amesema Mfuko pia unapata matokeo mazuri sana katika Uwekezaji hasa ukizingatia kuwa wanawekeza katika maeneo salama ambapo katika kipindi cha miaka miwili uwekezaji umeleta mapato makubwa.

"Ilikuwa haijafikiwa NSSF kuweza kupata mapato ya mwaka zaidi ya Shilingi bilioni 500 lakini katika mwaka huu wa fedha umepata zaidi ya Shilingi bilioni 600," amesema.

Alisema matokeo hayo ya uwekezaji yametokana na Mfuko kujikita zaidi katika uwekezaji kwenye maeneo ambayo yanaleta faida kwa Mfuko na kuhakikisha wanaudhibiti wa fedha.

Mshomba alisema chachu kubwa ya mafanikio ya NSSF imechagizwa na kasi ya utendaji wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa sababu amekuwa chachu ya ongezeko kubwa la wawekezaji hapa nchini hususan katika sekta binafsi.

"Tunamshukuru sana Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa chachu ya mafanikio ya Mfuko wetu kutokana na kufungua fursa za uwekezaji." alisema.

Kuhusu waajiri kutowasilisha michango amesema wameweka mikakati mbalimbali kwa kushirikiana na taasisi nyingine za Serikali ili kupata orodha kamili ya waajiri ambao watawafikia na kufuatilia michango ya wanachama.

Mshomba amewahamasisha Watanzania wote kushiriki katika zoezi zima la Sensa ya Watu na Makazi ifikapo tarehe 23 Agosti, 2022 ili waweze kuhesabiwa.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad