Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Mhe. Dk. Saada Mkuya (katikati), akizungumza na Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa (kushoto), na Mkuu wa Masoko
na Mawasiliano wa benki hiyo, Bi. Rahma Ngassa katika mkutano aliouandaa
akiwashirikisha wakuu wa taasisi mbalimbali za fedha za bara na
visiwani kujadili fursa mbalimbali za kifedha zipatikanazo katika
kampeni ya uchumi wa buluu iliyoasisiwa na Rais wa nane wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi. Hafla
hiyo ilifanyika visiwani humo jana. Uchumi wa Buluu ni dhana
inayohusisha uchumi unaojijenga katika Utalii, Uvuvi, Mafuta, gesi na
viwanda vinavyotumia malighafi za bahari.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa akizungumza huku wajumbe
wengine wakimsikiliza katika mkutano uliandaliwa na Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais, Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe.
Dk. Saada Mkuya (hayupo pichani), ukiwashirikisha wakuu wa taasisi
mbalimbali za fedha za bara na visiwani kujadili fursa mbalimbali za
kifedha zipatikanazo katika kampeni ya uchumi wa buluu iliyoasisiwa na
Rais wa nane wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi inayoendelea visiwani humo. Hafla hiyo ilifanyika
mjini Zanzibar jana. Uchumi wa Buluu ni dhana inayohusisha uchumi
unaojijenga katika Utalii, Uvuvi, Mafuta, gesi na viwanda vinavyotumia
malighafi za bahari.
Mkuu
wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya DCB, Rahma Ngassa akishiriki
pamoja na washiriki wengine mkutano uliandaliwa na Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais, Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk.
Saada Mkuya (hayupo pichani), ukiwashirikisha wakuu na wawakilishi wa
taasisi mbalimbali za fedha za bara na visiwani kujadili fursa
mbalimbali za kifedha zipatikanazo katika kampeni ya uchumi wa buluu
iliyoasisiwa na Rais wa nane wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi inayoendelea visiwani humo. Hafla
hiyo ilifanyika mjini Zanzibar jana. Uchumi wa Buluu ni dhana
inayohusisha uchumi unaojijenga katika Utalii, Uvuvi, Mafuta, gesi na
viwanda vinavyotumia malighafi za bahari.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya DCB, Godfrey Ndalahwa (katikati, akipozi katika
picha pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Dk. Saada Mkuya (wa tatu
kushoto) pamoja na wakuu na wawakilishi wa taasisi mbalimbali za fedha
kutoka bara na visiwani mara baada ya mkutano ulioandaliwa na mheshimiwa
waziri kujadili fursa mbalimbali za kifedha zipatikanazo katika kampeni
ya uchumi wa buluu iliyoasisiwa na Rais wa nane wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi
inayoendelea visiwani humo. Hafla hiyo ilifanyika mjini Zanzibar jana.
Uchumi wa Buluu ni dhana inayohusisha uchumi unaojijenga katika Utalii,
Uvuvi, Mafuta, gesi na viwanda vinavyotumia malighafi za bahari.
No comments:
Post a Comment