Msajili msaidizi mwandamizi Rehema Ludovick (Kulia,) akitoa huduma kwa mmoja wa wateja waliotembelea banda RITA katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea, Bi. Rehema amesema katika maonesho hayo watasajili na kutoa vyeti kwa wahitaji ambao hawajawahi kupata vyeti hivyo pamoja na kutoa elimu kwa Umma
Afisa Mawasiliano kutoka RITA Jafari Malema (Kulia,) akikagua baadhi ya nyaraka za mmoja ya wateja waliofika kusajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa kupitia maonesho ya kimataifa ya Sabasaba, Malema amesema wamejipanga kutoa huduma mbalimbali zinazotelewa na wakala hiyo ikiwemo kutoa elimu kwa Umma pamoja na kutoa msaada wa kisheria wa namna ya kuandika na kuhifadhi Wosia.
WAKALA Wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA,)
wameendelea kuwahudumia wananchi kwa kuwasajili na kuwapatia vyeti vya
kuzaliwa kwa gharama ya shilingi elfu kumi kwa kila mwombaji kupitia
maonesho ya kimataifa ya biashara maarufu kama Sabasaba yanayoendelea
jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
na waandshi wa habari katika maonesho hayo Afisa Mawasiliano kutoka
RITA Jafari Malema amesema kuwa, katika maonesho hayo ya kimataifa
wamejipanga kutoa huduma mbalimbali zinazotelewa na wakala hiyo ikiwemo
kutoa elimu kwa Umma pamoja na kutoa msaada wa kisheria wa namna ya
kuandika na kuhifadhi Wosia sambamba na masuala ya ndoa na talaka na
kubwa zaidi ni kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wananchi ambao
hawakuwahi kusajiliwa.
Amesema,
wamejipanga katika kuhakikisha wananchi wote watakaojitokeza wakati huu
wa maonesho wanapata vyeti vya kuzaliwa kwa wakati.
''Utaratibu
ni uleule tunaoufanya katika ofisi zetu wahitaji wa huduma hii
wanatakiwa kuja na viambatanisho au kielelezo kinachomtambulisha yeye,
Kama ni mtoto anatakiwa kuwa na aidha tangazo la kuzaliwa au kadi ya
kliniki pamoja barua ya Afisa mtendaji wa mtaa anapotokea, kwa mtu
mzima anaweza kuja na aidha tangazo la kuzaliwa kama analo, kadi ya
kliniki, cheti cha ubatizo, cheti cha kumaliza elimu ya
Msingi, kitambulisho cha utaifa au kadi ya kura pamoja na barua kutoka
kwa Afisa mtendaji wa mtaa anapotoka ili tuweze kupata taarifa zake na
sehemu anapotoka...Hapo atakuwa na sifa ya kusajiliwa na kupatiwa cheti
cha kuzaliwa kwa mujibu wa sheria.'' Amesema.
Aidha
amesema baada ya wananchii kusajiliwa wataalam watachakata taarifa hizo
na wahitaji kupewa vyeti vya kuzaliwa katika maonesho hayo ya Sabasaba
yanayoendelea kwa gharama ya shilingi elfu kumi kwa kila mwombaji bila
kigezo cha umri.
''Niwasihi
wananchi kufata kanuni na vigezo wakati huu wanapokuja katika maonesho
haya na kupata huduma katika banda la RITA,unapokuja kupata huduma
wahakikishe wanakuja na vielelezo vinavyoonesha wapi alipozaliwa, tarehe
aliyozaliwa na wazazi wake.'' Amesema.
Aidha
kuhusiana na watoto wasio na viambatanisho hivyo Malema amewashauri
wazazi kurudi mahali walipozaliwa ili kupata barua ya utambulisho na kwa
watoto wanaosoma kuna fomu maalumu ambayo wataiwasilisha katika shule
wanazosoma na Mwalimu mkuu kutoa taarifa ambayo Wakala hiyo itakuwa na
jukumu la kufuatilia katika Zahanati na hospitali walizozaliwa.
Kwa
upande wake Msajili msaidizi mwandamizi Rehema Ludovick amesema, katika
maonesho hayo watasajili na kutoa vyeti kwa wahitaji ambao hawajawahi
kupata vyeti hivyo pamoja na kutoa elimu kwa Umma juu ya masuala
mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kuandika na kuhifadhi Wosia na msaada wa
sheria kwa masuala ya ndoa na talaka.
Amesema kwa wahitaji waliozaliwa maeneo ya mipaka Wakala hiyo ipo tayari kuwasaida ili waweze kupata nyaraka hiyo muhimu.
''Kwa
waliozaliwa mikoa ya pembezoni ikiwemo Tarime, Kigoma, Namanga, Tanga-
Horohoro, Mpanda lazima wawe na viambatanisho vya wazazi na watapata
vyeti vyao baada ya kukidhi vigezo kwa kuwa ni haki ya kila mmoja wetu
na tupo hapa kwa ajili ya kuwasaida.'' Amesema.
Bi.
Rehema amewataka wananchi kutembeleea banda hilo ili waweze kupata
huduma na elimu kutoka kwa wataalam ambao wamepiga kambi katika viwanja
vya Sabasaba kwa kuwahudumia watanzania.
Baadhi
ya wananchi waliotembelea banda la RITA wamepongeza kasi na juhudi za
wataalamu wa Wakala hiyo katika kuwahudumia pamoja na kutoa elimu ambayo
watanzania wengi wanatakiwa wafahamu ili kila mmoja aweze kumiliki
nyaraka muhimu ya cheti cha kuzaliwa na kupata elimu juu ya umuhimu wa
kuandika na kuhifadhi Wosia pamoja na kupata msaada wa kisheria katika masula ya ndoa
na talaka.
Wananchi wakipata huduma.
Wananchi wakipata elimu na huduma katika banda la RITA katika viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment