KAMPUNI kinara ya Mafuta nchini TotalEnergies
imeendelea kuwafikia watanzania wenye malengo ya kumiliki vituo vya
mafuta kwa kuzindua kituo kipya cha mafuta Kigamboni jijini Dar es
Salaam, kituo hicho kinamilikiwa na kuendeshwa na mtanzania Mohammed
Salehe Affif aliyenufaika kupitia programu ya umiliki na uendeshaji
(DODO) huku ikielezwa kuwa kampuni hiyo itaendelea kutoa huduma bora kwa
watanzania pamoja na kushirikiana nao katika uwekezaji wa sekta hiyo
ili kujenga uchumi imara.
Akizungumza
mara baada ya kuzindua kituo hicho Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni
James Mkumbo amesema kuwa programu ya DODO inayoendeshwa na kampuni ya
TotalEnergies ya kushirikiana na wazawa imeleta kituo cha kwanza cha
mafuta cha TotalEnergies Kigamboni na kampuni hiyo ambayo huduma zake
zinafahamika kwa Umma kupitia ubora wake na viwango vya kimataifa.
''
Kwa niaba ya wananchi wa Kigamboni na Serikali kwa ujumla niwashukuru
TotalEnergies kwa kuendelea kuwafikia watanzania kwa kiwango kikubwa cha
umiliki wa vituo vya mafuta na kushiriki katika kujenga uchumi wa nchi
kupitia ubunifu, uwekezaji na ajira kupitia vituo hivi.'' Amesema.
Mkumbo
amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu
Hassan ameweka mazingira wezeshi ya uwekezaji yaliyopelekea mwekezaji
huyo mzawa kufanya uwekezaji mkubwa utakaowanufaisha wananchi wa
Kigamboni kwa kupata huduma na kutoa ajira kwa vijana wa maeneo jirani.
Aidha
amempongeza Mohammed Afiff kwa kuwawezesha wananchi wa Kigamboni kiushi
katika ndoto zao kwa kumiliki kituo kipya cha kisasa kitakachotoa
huduma kwa wakazi wa kigamboni na maeneo ya karibu na kutoa ajira kwa
vijana wa maeneo ya jirani.
Amesema
hiyo ni fursa kwa wananchi na wafanyabiashara wa Kigamboni kupata
huduma katika kituo hicho kwa kupata huduma za mafuta, kutengeneza
magari yao pamoja na kupata mahitaji mbalimbali kupitia duka la Bonjour
linalopatikana ndani ya kituo hicho kwa uhakika na usalama.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Biashara wa Vituo vya Mafuta vya
TotalEnergies Marieme Sav Saw amesema kuwa Wilaya ya Kigamboni imekuwa
ikikuwa kwa kasi kutokana na juhudi za Serikali za kuweka miundombinu
wezeshi ya kibiashara inayovutia uwekezaji ikiwemo daraja la Nyerere,
ujenzi wa barabara kutoka Ferry, Kibada na Kibada hadi Mwasonga hali
iliyopelekea mzawa huyo kuwekeza kwa manufaa ya wanakigamboni na
watanzania kwa ujumla.
Marieme
amesema kuwa mahusiano hayo ni hatua kubwa katika kuendeleza soko la
mafuta nchini na ni fursa kwa watanzania wenye maeneo na ndoto ya
kumiliki vituo vya mafuta kuitumia program ya DODO yenye uhakika wa
soko, mapato pamoja utambuzi kupitia chapa (brand,) ya TotalEnergies
yenye kutoa huduma bora na salama ikiwemo za mafuta bora (excellium
fuel) na vilainishi.
Pia
amesema kuwa ni fahari kwa TotalEnergies kufanya kazi na Mohammed Afiff
na wanawashukuru wateja wao kwa kuendelea kuwaamini na subira yavuta
heri kwa sasa wakazi wa Kigamboni watafurahia huduma zenye ubora na
viwango vya kimataifa.
Kwa
upande wake mmiliki na mwendeshaji wa kituo hicho Mohammed Afiff
amesema, amekuwa na ndoto ya kufanya kazi na kampuni ya TotalEnergies
kutokana na ubora wa huduma wanazozitoa na ubia huo wa kufanikisha
uzinduzi wa kituo hicho utanufaisha pia wakazi wa maeneo hayo kwa huduma
za mafuta na vilainishi, bidhaa kupitia duka la Bonjour pamoja na ajira
kwa wakazi wa maeneo hayo.
Awali
Meneja wa kuendeleza biashara kwenye vituo Thomas Meitaroni amesema,
kituo hicho kinachomilikiwa na mtanzania ni matokeo ya programu ya
umiliki na uendeshaji Dealer Owns, Dealer Operate, (DODO) programu
iliyobuniwa mahususi kwa wawekezaji wenye maeneo ya kujenga vituo vya
mafuta vyenye leseni halali zilizotolewa na mamlaka ya Tanzania kuingia
ubia na na kutumia chapa (brand) ya TotalEnergies.
Amesema
kupitia DODO wawekezaji wananufaika na kutumia nembo ya TotalEnergies
kampuni namba moja ya uuzaji mafuta na vilainishi nchini, soko la
uhakika kote nchini ambako vituo hivyo vimesambaa.
Uzinduzi
wa kituo hicho uliambatana na ofa maalum ambapo wateja walipata zawadi
mbalimbali na kubwa zaidi ni kupata punguzo la shilingi 50 kwa kila
lita ya mafuta waliyonunua.
Matukio mbalimbali wakati wa hafla ya ufunguzi wa kituo hicho.
No comments:
Post a Comment