Mkuu
wa Mkoa wa Songwe Omari Mgumba akutana na Maafisa wa Mamlaka wa
Mapato TRA na kuishukuru Mamlaka hio kwa kuwatembelea walipakodi hao wa
Mkoa wa songwe kwa ajili ya kutoa elimu mlango kwa mlango kufanya hivo
itapelekea uelewa mpana kwa wafanyabiashara wa Songwe kujua wajibu wa
mamlaka na wajibu wakulipakodi.
Pia
Mkuu wa mkoa aliendelea kwa kusema wafanyabiashara hao kutoa
ushirikiano wa dhati kwa ajili ya kupata elimu ya kodi, kwakuhakikisha
wasanimamia maneno na maelekezo ya Serikali ya Mh. Raisi wa Tanzania
Samia Suluhu Hassan bila kutumia nguvu, bila kutumia mabavu na bila
kutumia hila, Mamlaka ya Mapato imekua ikikusanya kodi kwa weledi
kukutana na wafanyabiashara kuwapa elimu ili kujua umuhimu wa kodi na
madhara ya ukwepaji kodiVilevile alitoa rai kwa wafanyabiashra wanapouza
bidhaa watoe risiti na mnunuzi kudai risiti kwa kutokufanya hivo
nikuikosesha mamlaka na serikali mapato yake halali na kudhoofisha
juhudi za serikali.
Kwa
upande wa Meneja wa Songwe wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw.
Dickson Kimaro aliongezea kwa kusema ujio wa Maafisa hao kutoka Makao
makuu utasaidia ongezeko la ukusanyaji wa mapato nakuondoa changamoto
walizokua nazo walipakodi katika mkoa huo wa Songwe.
Pia
Afisa uhusiano Mkuu Bw. MacDonald Mwakasindile kutoka Makao Makuu TRA
amesema kuwa kuwa zoezi hili linafahamika kwa jina la mlango kwa mlango
linalenga kuwahudumia wafanyabiashara ili kuangalia jinsi wanavyolipa
kodi.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Omari Mgumba akizungumza na maafisa wa TRA waliotembelea ofisini kwake kwa ajili ya kutoa elimu kwenye mkoa huo
Meneja TRA songwe Bw Dickson Kamaro
Afisa Uhusiano Mkuu Bw. macDonald Mwakasindile
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Bw. Omar Mgumba
No comments:
Post a Comment