HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Saturday, June 11, 2022

BENKI YA DCB YASHEREHEKEA MIAKA 20 YA MAFANIKIO KWA KUTOA FURSA ZA KIUCHUMI KWA WATANZANIA

 


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( kushoto ) akipokea tuzo ya shukrani ya Hayati Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ya huduma bora ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Uanzishwaji wa DCB ilikuwa moja ya ndoto za hayati Mkapa katika kuwasaidia wafanyabiashara ndogondogo waliokosa vigezo vya kupata mikopo ya mitaji kupitia mifumo rasmi ya kibenki. 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ) akikabidhi tuzo ya shukrani kwa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa benki hiyo, Edmund Mkwawa wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ) akikabidhi tuzo ya shukrani kwa Mwenyekiti wa Bodi Mstaafu wa benki hiyo, Prof. Lucian Msambichaka wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa  Katibu Muhtasi wa benki hiyo, Judith Maeda wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa  Ofisa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Rosemary Masaga wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ) akikabidhi tuzo ya utumishi wa miaka 20 kwa  Mhasibu wa Tawi wa benki hiyo, Prisca Donati wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa akizungumza na baadhi ya wanahisa wa benki hiyo na waalikwa wengine wakati wa hafla ya maadhimisho ya miaka 20 ya huduma bora ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Zawadia Nanyaro ( katikati ), aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza wa benki hiyo, Edmund Mkwawa ( kulia ), Katibu Muhtasi wa benki hiyo, Judith Maeda,  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Godfrey Ndalahwa, Mhasibu wa Tawi wa benki hiyo, Prisca Dona, Ofisa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Rosemary Masaga na Mwenyekiti wa Bodi Mstaafu wa benki hiyo, Prof. Lucian Msambichaka wakipiga picha ya kumbukumbu wakati wa Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Omar Kumbilamoto ( kulia ) akisalimiana na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Biashara ya DCB, Pamela Nchimbi wakati wa sherehe ya Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini leo. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Hanifa Suleiman Hamza na Mkurugenzi Mtendaji wa DCB, Godfrey Ndalahwa.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Banana Zoro akitumbuiza wakati wa Maadhimisho ya miaka 20 ya mafanikio ya benki hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad