HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, May 17, 2022

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUFUNGUA MAONESHO YA SABA YA WIKI YA UTAFITI NA UBUNIFU - UDSM

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa anatarajiwa kufungua Maonesho ya Saba ya wiki ya Utafiti na Ubunifu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 

Akizungumza na Wanahabari jijini Dar es Salaam, Naibu Makamu Mkuu wa wa Chuo (Utafiti) UDSM, Profesa Bernadetha Killian amewaalika watu wote kuweza kuhudhuria maonesho hayo ya siku mbili ambayo yatakuwa ya kipekee kwa mwaka huu.
Profesa Killian amesema kuwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kimejipanga vyema kufanya maonyesho hayo kuwa ya kipekee na mwaka 2022 wanaadhimisha miaka saba tokea kuanzishwa kwa maonesho hayo.

Maonesho ya Saba ya Wiki Ya Utafiti na Ubunifu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam yatakayofanyika rasmi Tarehe 24 hadi 26 Mei 2022, Katika Maktaba Mpya Ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad