HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 16, 2022

MKUU WA JESHI LA MAGEREZA, MEJA JENERALI SULEIMAN MZEE AZINDUA MIRADI YA MAENDELEO GEREZA UYUI, TABORA

KAMISHNA Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee mapema leo amezindua miradi ya Gereza Kuu Uyui,Tabora. Miradi hiyo ni mradi wa Duka, Mashine ya kusaga, majengo ya biashara. CGP Mzee amepongeza juhudi hizo za kumuunga mkono Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mema anayoyafanya kwa Jeshi na Taifa kwa ujumla.
KAMISHNA Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee mapema leo akikagua samani mbalimbali zinazotengenezwa katika Kiwanda cha Samani Uyui, Tabora. CGP Mzee amehimiza Kiwanda hicho kuzingatia maboresho hususani ubora na bei yenye uhalisia.
Baadhi ya Samani mbalimbali zinazotengenezwa na katika Kiwanda cha Samani Uyui, Tabora. Kiwanda hicho kipo Gereza Kuu Uyui.
Baadhi ya Maofisa na askari wa Gereza Kuu Uyui wakiwa timamu kwa ziara ya Mkuu wa Jeshi la Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee(hayupo pichani).
KAMISHNA Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee akiwasili Gereza Nzega kwa ziara ya kikazi mkoani Tabora. CGP Mzee amepongeza mabadiliko na juhudi za maendeleo ya ujenzi wa nyumba za makazi katika Gereza la Nzega.
Ujenzi wa nyumba za makazi ya askari Gereza Nzega, Tabora ukiendelea katika hatua za awali(msingi) kama inavyoonekana pichani.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee akikagua nyumba za askari Gereza Uyui, Tabora.
Muonekano wa nyumba za maafisa na askari wa Gereza Kuu Uyui, Tabora.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Meja Jenerali Suleiman Mzee(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na askari wa Gereza Kuu Uyui, Tabora mara baada ya kutembelea Gereza hilo leo Mei 16, 2022. Picha zote na Jeshi la Magereza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad