Na. Damian Kunambi, Njombe
Ikiwa
tunaelekea mwezi wa sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika
Agosti 23 mwaka huu kote nchini Wilaya ya Ludewa iliyopo mkoani Njombe
imeunda timu zitakazo ongozwa na viongozi wakuu wa wilaya hiyo ambazo
zitapita na kutoa elimu katika kata zote 26 za Wilaya ya Ludewa ili
kuhakikisha kuwa zoezi hilo linafanikiwa kikamilifu.
Akizungumza
katika kikao cha Kamati ya Sensa wilayani humo mkuu wa Wilaya ya Ludewa
Andrea Tsere amesema sanjari na kupita katika kata hizo lakini pia
watatumia viongozi wa dini mbalimbali ili waweze kuelimisha waumini wao
katika nyumba za ibada.
"Viongozi
wa dini na madhehebu yote tutawaomba watangaze wao wenyewe suala la
Sensa tena ikiwezekana wanukuu baadhi ya vifungu vilivyopo katika vitabu
vya dini, ambavyo vinaelezea zoezi la kuhesabu watu".
Aidha
kwa upande wa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Sunday Deogratius amesema
ili kuweza kufanikisha zoezi hilo wanapaswa kujitoa hivyo tayari ofisi
yake imefanya maandalizi ya magari kwaajili ya kusafirisha timu hizo.
"Tunapaswa
kujitoa na kujigawa kwa makundi ili kazi yetu iweze kwenda vizuri, mimi
nitatoka na kundi langu, mkuu wa wilaya atatoka na kundi lake vivyo
hivyo kwa mwenyekiti wa Halmashauri na tutasambaa maeneo tofauti tofauti
ya wilaya hii".
Aidha
kwa upande wa mmoja wa wanakamati wa kikao hicho Thomas Kiowi ambae ni
Afisa maendeleo ya jamii alitoa mapendekezo ya kufikisha elimu hiyo
mapema kwa baadhi ya kata za tarafa ya mwambao ambako asilimia kubwa ya
wakazi wake ni wavuvi na wanakawaida ya kusafiri maeneo mbalimbali
kwaajili ya shighuli hizo za uvuvi huku Alex Henjewele ambaye ni mratibu
wa Sensa wilayani humo amesema zoezi hilo litafanyika kwa muda wa siku
10.
Pamoja
na mikakati hiyo ya kufanikisha zoezi hilo la sensa, lakini bado
kumeonekana kuwepo kwa baadhi ya changamoto ya kimiundombinu katika
maeneo ya tarafa za mwambao na kwingineko ambapo watalazimika kupita
kwenye mapori kwa kutembea kwa miguu kutokana na kutokuwa na barabara
huku wakazi wake wakiushi mbalimbali.
No comments:
Post a Comment