HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Sunday, April 3, 2022

Benki ya CRDB ilivyoshiriki hafla ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan

Mufti wa Tanzania Dk. Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ali (kushoto), akipongezwa na Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al-Barakah Banking, Rashid Rashid, wakati wa hafla fupi ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan pamoja na kumpongeza kwa kutunukiwa Shahada ya udaktari wa heshima (PHD) na Chuo Kikuu cha nchini Gambia.  (Na Mpigapicha Wetu).

Mufti wa Tanzania Dk. Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ali (kushoto), akizungumza katika hafla fupi ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan pamoja na pongezi kwa kutunukiwa Shahada ya udaktari wa heshima (PHD) kutoka Chuo Kikuu cha nchini Gambia. 
Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al-Barakah Banking, Rashid Rashid, akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan pamoja na kumpongeza Mufti wa Tanzania Dk. Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ali kwa kutunukiwa Shahada ya udaktari wa heshima (PHD) na Chuo Kikuu cha nchini Gambia.  
Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al-Barakah Banking, Rashid Rashid, akizungumza na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake BAKWATA, Shamim Khan.
Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al-Barakah Banking, Rashid Rashid (wa pili kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dk. Alhad Mussa Salum (kushoto kwake) wakati wa hafla ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan pamoja na kumpongeza Mufti wa Tanzania Dk. Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ali kwa kutunukiwa Shahada ya udaktari wa heshima (PHD) na Chuo Kikuu cha nchini Gambia.
Wateja wa Benki ya CRDB wakifungua akaunti ya CRDB Al-Barakah Banking.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad