HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, February 24, 2022

Wadhibiti Waandamizi wa Sekta ya Kifedha kutoka taasisi mbalimbali duniani watoa heshima kwa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Benno J. Ndulu, na kuahidi kuendeleza maono yake.

 Katika kumuenzi marehemu, Benno Ndulu, baadhi ya viongozi wa benki kuu za Afrika

walikusanyika katika kikao kilichoendeshwa mtandaoni siku ya Jumanne tarehe 22 Februari

pamoja na familia ya Prof. Ndulu na jamaa kutoka nchi mbalimbali duniani kuadhimisha dira

yake ya kipekee ya kiuchumi wa Afrika.

“Leo ni mwaka mmoja tangu tumpoteze shujaa wetu. Msomi mashuhuri, mchumi mahiri wa

maendeleo, mwanabenki mwenye maono, mchambuzi wa masuala ya kifedha, mtu mashuhuri,

na mtu wa vitendo. Huyu ndiye Profesa Benno Joseph Ndulu.”

Ndivyo alivyosema Prof Florens Luoga aliyemrithi Prof. Ndulu kuwa Gavana wa Benki Kuu ya

Tanzania.

Hafla hii iliandaliwa na FINSYS, wataalamu wa ushauri wa maendeleo ya sekta ya kifedha, na

kuongozwa na Prof. Njuguna Ndung’u, Mkurugenzi Mtendaji wa African Economic Research

Consortium. Profesa Ndulu alikumbukwa sana na wazungumzaji mashuhuri wa Kiafrika akiwemo

Prof. Luoga, mwanauchumi wa Uganda Dk Louis Kasekende na Gavana wa Benki ya Hifadhi ya

Afrika Kusini Lesetja Kganyago. Prof. Ndung’u alitoa maoni yake:

"Inapendeza kuona jumuiya mashuhuri ikiungana pamoja kumkumbuka rafiki yetu mkubwa, na

kuchunguza jinsi ya kuendeleza maono yake."

Aidha, tukio hilo halikuwa ukumbusho tu. Wazungumzaji waliangazia jinsi ya kutimiza maono ya

Prof. Ndulu, ikiwa ni pamoja na African Continental Free Trade Agreement (AfCFTA), sana sana

katika kuendeleza miundombinu ya malipo ya kikanda ya gharama nafuu na ya haraka – Shauku

ya Profesa Ndulu.

Dk Kasekende alieleza umuhimu wa kuimarisha malipo ya Afrika:

"Moja ya michango ya kipekee ya Profesa Ndulu ilikuwa kutambua umuhimu wa kuchochea

ukuaji kupitia biashara ya kikanda na ndani ya bara. Biashara ya ndani ya Afrika inawakilisha

16.6% tu ya biashara zote za kuvuka mpaka za Afrika; kuongeza hii itakuwa na faida kubwa za

kiuchumi kwa Afrika. Aliona maendeleo ya malipo ya mipakani kama sababu moja muhimu

katika kuunga mkono dira hii, na akaanzisha maendeleo ya muda mrefu ya miundombinu ya

malipo ya Tanzania na kikanda.”


1


Kama Gavana Kganyago alivyoona,

“Bara letu ni miongoni mwa mabara yenye malipo ghali zaidi duniani. ...Mifumo mipya ya

malipo ya kuvuka mipaka itahitaji uratibu wa kimataifa na usaidizi wa kisiasa na [hii] itategemea

sana sekta ya umma na ya kibinafsi kushirikiana. Hatuthubutu kushindwa katika jitihada hii.”

Katika mtazamo wa kimataifa, maono haya ya Kiafrika yaliungwa mkono kwa nguvu,

ikithibitishwa na michango kutoka kwa Prof. Klaas Knot, Mwenyekiti wa Bodi ya Financial

Stability Board (FSB), ambaye alielezea Mwongozo wa FSB wa kuimarisha malipo ya mipakani na

kazi inayoendelea ya kutambua fursa maalum za uboreshaji.

Kulingana na Prof. Knot:

"Mafanikio ya yatategemea ushirikiano wa umma na sekta binafsi, uratibu wa mifumo ya

udhibiti na usimamizi, uelewa wa miundombinu ya mifumo ya malipo iliyopo na upunguzaji wa

gharama na kuboresha usindikaji wa data."

Huku FSB imeweka dhamira yake katika kuleta mabadiliko ya kweli kwa watu binafsi, biashara na

sekta za kifedha duniani kote. Bara la Afrika linanafasi ya kufanikiwa zaidi kutokana na utimizaji

wa malengo haya ya kimataifa kwani bado kuna changamoto za gharama, urahisi na uharaka wa

upatikanaji wa huduma za kifedha.

Gerard Hartsink, Mwenyekiti wa zamani wa Baraza la Malipo la Ulaya, alichangia uzoefu wa

Ulaya katika kuunda Single Euro Payments Area (SEPA) (mfumo wa malipo katika nchi za Ulaya),

akisisitiza uongozi thabiti kutoka benki kuu na ushiriki wa sekta kibinafsi. Wazungumzaji wote

wawili walisisitiza uwiano wa maendeleo ya kimataifa na mtazamo wa Kiafrika wa Prof. Ndulu.

Prof. Luoga alieleza mantiki ya msingi ya malipo ya gharama nafuu, haraka, jumuishi na ya

uwazi:

"Profesa Ndulu aliamini katika kuwawezesha watu maskini, hasa kwa kupata huduma za kifedha

kama njia ya kupambana na umaskini. Katika kufanikisha hili, ushirikishwaji wa kifedha ulitawala

Ugavana wake ambao uliiwezesha Tanzania kutoka katika hali duni na kufikia mojawapo ya nchi

zinazoongoza barani Afrika.”

Katika kutimiza ndoto ya Profesa Ndulu, Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

iliitisha kongamano katika utekelezaji wa majukumu yake chini ya Kifungu cha 26 cha Mkataba

wa Eneo Huria la Biashara linalozitaka wanachama wa EAC, COMESA, na SADC kushirikiana na

kuimarisha uratibu katika masuala yanayohusu mifumo ya malipo. Kongamano lilijadili chaguzi

za kuimarisha mipango ya malipo ya rejareja ili kuboresha biashara ya mipakani. Uongozi wa

Benki Kuu za nchi mbalimbali katika EAC, SADC, COMESA unapaswa ushughulikie haraka

mapendekezo yanayotokana na kongamano hilo.

Prof. Njuguna Ndung’u
Prof. Florens Luoga
Dr. Louis Kasekende
Prof. Dr. Klaas Knot
Mr. Lesetja Kganyago
Gerard Hartsink
Hon. Dr. Peter Mathuki

 














No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad