HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, January 19, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa atembelea miradi mbalimbali mjini Sumbawanga

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti (aliyevaa kofia nyeusi) akitazama kituo cha kuchotea maji ambacho hakifanyi kazi jana alipokagua  zahanati ya kijiji cha Fyengeleza Manispaa ya Sumbawanga na kuagiza wataalam wa Ruwasa kukamilisha mradi huo ili wananchi wapate maji. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya.
Tanki la maji lenye uwezo wa kuhifadhi lita 150,000 za maji lililokamilika katika mradi wa waji wa kijiji cha Mponda Manispaa ya Sumbawanga chini ya usimamizi wa RUWASA .
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti (aliyevaa shati la kitenge) akitazama tanki la maji lililojengwa na RUWASA Sumbawanga kwa ajili ya mradi wa maji kijiji cha Mponda ambapo watu zaidi ya 1800 watanufaika ambapo mradi huo umegharimu shilingi Milioni 240.


Mkazi wa kijiji cha Fyengeleza Jacklina Masanja (mwenye mtoto kushoto) akizungumza kushukuru serikali kwa kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho jana wakati Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti (aliyevaa kofia nyeusi) alipotembelea kuona huduma kituoni hapo.
Meneja wa TARURA Sumbawanga Mhandisi  Samson Kalesi (kushoto ) akitoa maelezo ya ujenzi wa barabara ya lami ya Petrol Station- High Court yenye urefu wa kilometa moja jana wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ( aliyevaa kofia nyeusi) jana mjini Sumbawanga

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad