Na Amiri Kilagalila,Njombe
JUMUIYA
 ya umoja wa wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Njombe,imefanikiwa 
kutekeleza agizo la Chama ngazi ya taifa kwa kujenga nyumba za watumishi
 ili kupunguza changamoto za watumishi wa Jumuiya wanapokuwa wamepanga 
mitaani.
Akizungumza
 baada ya kukagua nyumba hiyo iliyopo mtaa wa Nzenge halmashauri ya mji 
wa Njombe,Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Njombe Scolastika Kevela,amesema 
jumuiya hiyo wilaya ya Njombe imeonyesha mfano kwa wilaya zote za mkoa 
huo na taifa kwa kutekeleza agizo kwa wakati na kuahidi kuendelea 
kumuunga mkono mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi taifa kwa vitendo.
“Kwanza
 niwapongeze UWT wilaya ya Njombe kwa kazi kubwa mliyoifanya,hili ni 
agizo kutoka taifa kwamba tuhakikishe mkoa na wilaya zote tunajenga 
nyumba za watumishi wa jumuiya ili kupunguza changamoto za 
kupanga”alisema Scolastika Kevela
Ameongeza
 kuwa mkoa wa Njombe utaenedelea kuwa bega kwa bega na mwenyekiti wao wa
 Chama taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
“Njombe
 tuko bega kwa bega na Samia Suluhu na 2025 Njombe tutakuwa na jambo 
letu na tutaendelea kumuunga mkono kwa vitendo na huu ndio utendaji 
unaoonekana”alisema Kevela
Naye
 mwenyekiti wa jumuiya hiyo wilaya ya Njombe Betrece Malekela,amesema 
agizo hilo lilitolewa tarehe 23 ya mwezi wa 9 wakiwa Rufiji na kupata 
hamasa kubwa ili kumailisha nyumba hiyo kwa wiki tatu pekee na kuwa 
miongoni mwa wilaya chache nchini zilizotekeleza agizo hilo.
“Tulipata
 hamasa na tukatii maagizo maana ilionekana ni nyumba chache 
zilizojengwa kwa nchi nzima,nyumba hii imekamilika ndani ya wiki tatu 
wala sio kitu kidogo”alisema Betrece Malekela
Wajumbe
 wa baraza la UWT mkoa wa Njombe waliofika na kukagua nyumba 
hiyo,wamesema ukamilishaji wa nyumba hiyo umetokana na umoja walio nao 
na wilaya ya Njombe imekuwa ni mwanga na kutoa hamasa kwa wilaya 
nyingine kutekeleza agizo hilo.
Mwenyekiti
 wa UWT mkoa wa Njombe Skolastika Kevela pamoja na wajumbe wa baraza 
wakikagua idadi ya vyumba na muonekano wa ndani wa nyumba hiyo iliyopo 
mtaa wa Nzenge.

No comments:
Post a Comment