HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Thursday, December 30, 2021

TICTS WAIPIGA SOP SOP COCO BEACH, DAR ES SALAAM

Wafanyakazi wa Kampuni ya Kimataifa ya kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumaliza kufanya usafi katika fukwe za Coco Beach, Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono zoezi la Usafi katika jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na Uongozi wa Serikali ya mtaa wa Oysterbay kupitia kampeni yao ya "Go Green", lililofanyika leo Desemba 30, 2021. Wafanyakazi hao waliongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wao, Horace Hui.
 
BOFYA HAPO CHINI KUONA VIDEO
 
 
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Kimataifa ya kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS) wakiendelea na usafi usafi katika fukwe za Coco Beach, Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa ya  kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS),Horace Hui (kushoto) akimkabidhi sehemu ya miti, Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Oysterbay, Anna Malisha, ikiwa ni  sehemu ya kuunga mkono serikali ya mkoa wa Dar es salaam ya kufanya usafi na kupanda miti katika mazingira yanayowazunguka wananchi kutipia kampeni yao ya "GO Green", kabla ya kuanza kwa zoezi la usafi katika fukwe ya Coco Beach, leo Desemba 30, 2021. kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS, Donald Talawa.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa ya  kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Horace Hui (kushoto) akimkabidhi sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi, Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Oysterbay, Anna Malisha, ikiwa ni  sehemu ya kuunga mkono serikali ya mkoa wa Dar es salaam ya kufanya usafi katika mazingira yanayowazunguka wananchi kutipia kampeni yao ya "GO Green", kabla ya kuanza kwa zoezi la usafi katika fukwe ya Coco Beach, leo Desemba 30, 2021. kulia ni Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS, Donald Talawa.
Vifaa vya usafi vilivyotolewa kwa ajili ya kuunga zoezi la usafi jiji la Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kimataifa ya  kuhudumia Makontena Tanzania katika bandari ya Dar es salaam (TICTS), Horace Hui (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS Donald Talawa (kulia) wakifanya usafi katika fukwe za Coco Beach, Dar es Salaam ikiwa ni kuunga mkono zoezi la Usafi katika jiji la Dar es Salaam kwa kushirikiana na Uongozi wa Serikali ya mtaa Oysterbay kwenye zoezi la kufanya usafi lililopewa jina la (GO Green) kwenye fukwe ya Coco Beach.
Wafanyakazi wa Kampuni ya TICTS wakiendelea na usafi usafi katika fukwe za Coco Beach, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad