HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Monday, December 13, 2021

CSI ILIVYOUTUMIA MWAKA 2020/2021 KUWASHIKA MKONO WANANCHI PAMOJA NA VIJANA WA TANZANIA KATIKA KUTIMIZA NDOTO ZAO


Uogozi wa Shirika la Childbirth Survival International(CSI) wakiwa kwenye picha ya pamoja na walimu wa Chuo cha Urembo Maznat pamoja na washiriki waliofika kwenye usaili wa kuwapata vijana wawili uliofanywa chini ya CSI na Chuo cha Urembo cha Maznat .

Na Said Mwishehe, Michuzi TV
SHIRIKA la Childbirth Survival International(CSI) tangu kuanzisha kwake miaka 10 iliyopita limefanya mambo makubwa hasa katika eneo la kupunguza vifo vya mama mjazimto na watoto chini ya miaka mitano.
Aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani ambaye kwa sasa ni Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Tanzania, Balozi Liberata Mulamula(kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwanzilishi wa Shirika la Childbirth Survival International(CSI)Tausi Hamis Kagasheki(kulia) alipokuwa ametembelea banda la Shirika ilo nchini Marekani

Hata hivyo kwa mwaka huu wa 2021 limefanya mambo mbalimbali katika jamii ya Watanzania na moja ya kazi hizo ni uamuzi wake wa kuwa na programu maalum ya kuwasaidia vijana kiuchumi kwa kufanikisha ndoto zao.

Kupitia programu hiyo CSI ilijikita katika kuwatafuta vijana wenye ndoto na kisha kuzifanikisha.Hivyo ilibeba jukumu, kwanza la kuwatafuta vijana wenye ndoto kupitia kongamano maalumu lililofanyika Mombasa jijini Dar es Salaam, na baada ya hapo vijana waliopatikana walipatiwa nafasi ya kupelekwa Chuo cha Urembo Maznat na kulipia gharama zote, kuanzia ada ya masomo hadi nauli za usafiri wa kwenda na kurudi kwa muda wote wa masomo.
Madakatari kutoka hospitali mbalimbali za Jijini Dar es Salaam wakiendelea na kazi ya kuwachunguza watoto Njiti kwa ajili a kujua afya zao ili kuwaepusha na magonjwa mbalimbali yanayoweza kuwakabili wakati wa zoezi la kutoa huduma za kiafya kwa watoto njiti iliyoandaliwa na Dorris Mollel Foundation na kufanyika katika ukumbi wa Don Bosco jijini Dar es Salaam.

Ukweli programu hiyo ya CSI kwa mwaka 2021 imebadilisha maisha ya vijana wengi, hata wale ambao hawakubahatika kuchaguliwa, kuanzia hapo walibadili mitazamo yao na kuona kumbe wanaweza kutimiza ndoto zao kwa kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
Hivyo wakati mwaka 2021 unakwenda kumalizika, vijana wanabakia na kumbukumbu nzuri namna CSI ilivyowashika mkono kwa vitendo, iliona haja ya kuwabeba na kufanikisha ndoto zao.

Baadhi ya vijana waliobahatika kupata nafasi ya kufadhiliwa masomo na CSI wamesema 2021 unabakia kuwa mwaka wa kumbukumbu kubwa katika maisha yao itakayochukua miaka mingi kufutika.
Kwa kukumbusha tu programu ya kuwasaidia vijana ilianza Januari mwaka 2021 na katika kongamano la kuwatafuta vijana kwa ajili ya kuwasaidia walijitokeza zaidi ya 100 na kati ya hao wawili wakabahatika kupata ufadhili wa masomo.

CSI imefanya hivyo kwa kuamini vijana ndio wazazi wa kesho , na wakiwezeshwa kiuchumi itakuwa rahisi kumudu kuhudumia familia zao, hivyo kupunguza changamoto za kimaisha zikiwemo za kumudu gharama za matibabu ya afya hasa kupunguza vifo kwa mama mjawazito na mtoto.
David Francis ambaye aliibuka mshindi kwenye usaili wa kuwapata vijana wawili uliofanywa chini ya CSI na Chuo cha Urembo Maznat akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna alivyojiamini mpaka kuwa mshindi kwenye shundano hilo.

David Francis Matongo ni mmoja ya wanufaika wa mradi wa kusaidia vijana , hivyo anasema mwaka 2021 kwake umekuwa wenye bahati kubwa , ndio mwaka uliomkutanisha na CSI inayoongozwa na kusimamiwa na wamama wawili wema wenye nia ya kusaidia wengine.

"Nikiri mwaka 2021 umenikutanisha na CSI, umenikutanisha na watu wema ambao kwa kweli wamebadilisha maisha yangu. Ndoto yangu ya muda mrefu ilikuwa ni kujifunza urembo , nashukuru CSI wameifanya itimie katika mwaka huu,"amesema.
Meneja wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival International(CSI) Ester Mpanda pamoja na wanafunzi wakipata maelekezo kutoka kwa uongozi wa Chuo cha Urembo Maznat mara baaada ya kuwasili chuoni hapo kwa ajili ya kuanza masomo ya urembo

Anaeleza anakumbuka Januari 2021 CSI walitafuta vijana."Tulikuwa wengi siku ile na mimi nikabahatika, Februari 19 nilianza masomo Chuo cha Urembo Maznat, tuligharamiwa kila kitu na CSI."
David anasema CSI imenisaidia kutimiza ndoto zake na sasa anaweza kumudu maisha yake, kupitia ujuzi ambao ameupata amekuwa akifanya shughuli zake na kumuingia kipato."Mwaka 2021 kwangu unabakia kuwa mwaka mzuri,ahsanteni CSI kwa wema wenu huu."

Wakati anazungumza na Michuzi Blog na Michuzi TV katika mwaka huu, David ameweka wazi ambavyo sasa anaweza kupamba bibi harusi, kupamba majukwaa, kutengeneza kucha, kufanya masaji , kusuka na kufanyia mtu make Up.Yote hayo amejifunza kwa ufadhili wa fedha za CSI.
Meneja wa Programu za Vijana katika shirika la Childbirth Survival International(CSI) Ester Mpanda akizungumza na washiriki wakati wa mchakato wa kuwapata vijana hao kupitia usaili uliofanywa chini ya CSI na Chuo cha Urembo Maznat ili kuwapata vijana wawili watakaofadhiliwa na shitika hilo kwenye masomo ya urembo.

Kwa upande wake Meneja Programu za Vijana wa CSI Ester Mpanda wakati anazungumza siku walipozindua programu hiyo alieleza wazi CSI wanaamini unapomuandaa kijana wa leo katika kutimiza ndoto yake kimaisha, maaa yake unamsaidia kiuchumi.
Madakatari kutoka hospitali mbalimbali za Jijini Dar es Salaam wakiendelea na kazi ya kuwachunguza watoto Njiti kwa ajili a kujua afya zao ili kuwaepusha na magonjwa mbalimbali yanayoweza kuwakabili wakati wa zoezi la kutoa huduma za kiafya kwa watoto njiti iliyoandaliwa na Dorris Mollel Foundation na kufanyika katika ukumbi wa Don Bosco jijini Dar es Salaam.

"Kwa muda wote CSI tunaendelea kutimiza majukumu yetu kwa kushirikiana na Serikali, kwetu sisi tunajisikia fahari kuona takwimu zinaonesha vifo vya mama mjamzito na watoto chini ya miaka mitano vikiendelea kupungua.Pamoja na hayo tumeona haja ya kuwasaidia vijana kupitia programu hii."
Kuhusu CSI, ni shirika la kimataifa ambalo limeanzishwa na wamama wa wawili Tausi Hamis Kagasheki anayeishi nchini Marekani ambako ndiko yalipo makao makuu ya CSI pamoja na Mama Stella Mpanda anayeishi nchini Tanzania.

Wamama hao jasiri waliamua kuanzisha shirika hilo ikiwa ni mkakati wa kukabiliana au kupunguza vifo kwa mama mjazito na mtoto wakati wa kujifungua.Ukweli wamefanikiwa kwa kiwango kikubwa.Kwa kutambua thamani ya uhai waliamua kupanua wigo, hivyo CSI , na zaidi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao katika nchi nyngine .
Meneja wa Programu za Vijana kutoka CSI, Ester Mpanda, timu ya Shirika la Childbirth Survival International(CSI) pamoja na timu ya Dorris Mollel Foundation wakiwafanyia usajili mama na mtoto waliofika kwa ajili ya watoto Njiti kufanyiwa uchunguzi na madaktari kutoka hospitali ya Muhimbili, Aga Khan na kuandaliwa na Dorris Mollel Foundation iliyofanyika Don Bosco jijini Dar es Salaam

Kupitia CSI wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii kuhusu kutambua afya ya uzazi salama kupitia programu mbalimbali ambazo wamekuwa wakizitoa kwa zaidi ya miaka 10 sasa sambamba na kusaidia vifaa vya kujifungulia katika hospitali mbalimbali nchini. 
Mbali ya Tanzania, CSI ipo pia katika nchi za Somalia, Rwanda, Uganda, Marekani, na wanarajia kuwa na tawi nchini Burundi pamoja na Kenya kwa nchi za Afrika Mashariki.

Meneja wa Programu za Vijana Shirika la Childbirth Survival International(CSI) CSI, Ester Mpanda akizungumza kuhusu CSI Tanzania inavyoshirikiana na Doris Mollel Foundation wakati wa maadhimisho Siku ya Mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba 17 ya kila mwaka yaliyofanyika katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad