HABARI MPYA

Home Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, December 14, 2021

BALOZI MULAMULA ASHIRIKI MAADHIMISHO YA MT. LUCIA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula ashiriki katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia iliyoandaliwa na Ubalozi wa Sweden hapa nchini. Mbali na Balozi Mulamula, Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo pia alishiriki katika hafla hiyo iliyofanyika jana jioni jijini Dar es Salaam.


Badhi ya watoto wakiimba nyimbo maalum ya kumbukizi ya Mtakatifu Lucia 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akipokea zawadi ya picha kutoka kwa Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia. Sherehe hiyo iliandaliwa na  Ubalozi wa Sweden.




Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiteta jambo na Mbunge wa Urambo (CCM), Margreth Sitta katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akijadili jambo na Balozi wa Norway Mhe. Elisabeth Jacobsen pamoja na Balozi wa Denmark nchini, Mhe. Mette Norgaard Spandet katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akijadili jambo na Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg pamoja na Balozi wa Norway Mhe. Elisabeth Jacobsen  


Balozi wa Denmark nchini, Mhe. Mette Norgaard Spandet akifurahia jambo na Mbunge wa Urambo (CCM), Margreth Sitta pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula, Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo pamoja na viongozi wengine akiwemo Mbunge wa Urambo Magreth Sitta wakifuatilia sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia


Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg akiongea na viongozi mbalimbali walioshiriki katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Anders Sjöberg katika sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia 

Badhi ya watoto wakiimba nyimbo maalum ya kumbukizi ya Mtakatifu Lucia 


Badhi ya viongozi wakishuhudia sherehe za maadhimisho ya Mtakatifu Lucia 


    Maadhimisho ya Seherehe ya Mtakatifu Lucia yakiendelea  


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad