Waziri
wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Jamal Kassim Ali akisoma
hotuba ya ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya huduma za Fedha Kitaifa
alipokuwa anafungua maonesho hayo yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi
Mmoja kuanzia tarehe 08 na hadi tarehe 14 Novemba 2021 yenye lengo la
kuwakutanisha wadau mbalimbali na kutoa elimu Juu ya huduma za Fedha.
Na Mwandishi Wetu
Bodi
ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania(NBAA) imeshiriki
maonesho hayo ya Wiki ya huduma za Fedha Kitaifa ili kuongeza uelewa kwa
wananchi kuhusu kazi na huduma mbalimbali zinazotolewa na Bodi. Kauli
mbiu ya maonesho hayo ni “Boresha Maisha kupitia elimu ya fedha.”
Maadhimisho ya wiki ya huduma za Fedha Kitaifa yameandaliwa
na Wizara ya Fedha na Mipango yaliyoanza tarehe 08 na hadi tarehe 14
Novemba yenye lengo la kuwakutanisha wadau mbalimbali na kutoa elimu Juu
ya huduma za Fedha.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,
Fedha na Mipango, Jamal Kassim Ali amesema Serikali imepanga kutumia
Fedha kwanye mitaji ya wajasiariamali wadogowadogo ambao wanatoa huduma
za kifedha kwenye Mpango wa Maendeleo ya sekta ya Fedha hapa nchini.
Amesema
Elimu ijikite kwenye huduma za Fedha ili waweze kukuza kipato cha mtu
mmojamoja na kuongeza mapato kwa taifa hivyo ni vyema kujipima ipasavyo
ili kuongeza ufanisi kwenye huduma za kifedha hapa nchini.
Akizungumza
kwenye maonesho hayo Afisa Masoko na Mawasiliano wa Bodi ya Taifa ya
Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), Magreth Kageya amesema
unapozungumzia huduma za Fedha huwezi kumwacha Mhasabu na Mkaguzi kwani
wao ndio waandaaji na Wakaguzi wa Hesabu za Fedha.
Mwisho
amewakaribisha wananchi na wadau wote wa Taaluma ya Uhasibu kutembelea
banda lao katika viwanja vya Mnazi Mmoja ili kupata elimu zaidi juu ya
kazi na huduma mbalimbali zinazotolewa na NBAA.
Afisa
Masoko na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya akitoa maelezo kwa Ngabo
Nyamaseki kuhusu kazi zinazofanywa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na
Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) kwenye maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam leo.
Afisa
Masoko na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya akitoa maelekezo kuhusu
huduma mbalimbali zinazotolewa na NBAA kwenye Maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam leo.
Afisa
Masoko na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya akitoa maelezo kwa Franco
Kakurwa kuhusu gharama za mitihani ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na
Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) kwenye maonesho ya Wiki ya Huduma za
Fedha Kitaifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es
Salaam leo.
Afisa
Masoko na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya akitoa maelezo kwa Japhet
Muluma namna anavyoweza kujiunga na Mitihani ya Bodi ya Taifa ya
Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) hata kama hajasomea
taaluma ya Uhasibu kwenye maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa
yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam leo.
Maonesho yakiendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jijjini Dar es Salaam
No comments:
Post a Comment