Akizungumza
 katika eneo la mradi, Bi, Nasombe amesema endapo mvua za vuli 
zitanyesha kabla mfereji mkuu wenye urefu wa mita ELFU TATU NA MIANNE 
(Mita3,400) kusakafiwa athari kubwa zinaweza kujitokeza ikiwemo maji 
kubadili mwelekeo na kuvamia makazi ya watu kwa sababu ya mlundikano wa 
udongo uliochimbwa kwaajili ya ujenzi wa Mfereji Mkuu unaoweza pia 
kufukiwa kutokana na mvua zinazotarajiwa kunyesha hivi karibuni.
Kwa
 upande wake Mhandisi Juma Hamsini wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji 
amemshauri mkandarasi kuwashirikisha Wataalam wa Halmashauri, wanakijiji
 wa Kirya na viongozi wa maeneo mradi unapotekelezwa kwa kuwa wanaijua 
Geografia ya eneo husika na mazingira yanayowazunguka, suala 
litakalomsaidia mkandarasi katika kutekeleza wajibu wake wakati huu wa 
ujenzi.
Mnufaika
 wa Mradi huo ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya ujenzi Bw, Nyange Laizer
 ameishukuru serikali kwa mradi huo utakaoboresha maisha ya wafugaji 
katika kijiji cha Kirya kwa kuongeza pato la familia kupitia kilimo cha 
Umwagiliaji.
Mhandisi
 Msimamizi wa Mradi huo kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Romwald 
Robert, amekiri mkandarasi kuwa nyuma ya muda uliopangwa kwa mujibu wa 
mkataba ambapo ameahidi kumsimamia kwa karibu mkandarasi huyo na 
kumshauri ili aweze kutekeleza majukumu yake kwa kasi na kufidia muda 
ulipotea hatimaye mradi huo ukamilike katika muda uliopangwa.
Ujenzi
 wa Mfereji Mkuu utawezesha Banio la pili kuanza kufanya kazi na 
kuongeza eneo la Umwagiliaji kutoka Hekta Mia nne Hamsini (Hekta 450) 
hadi Hekta Miatisa (Hekta 900) ambapo ujenzi huo unajumuisha barabara 
yenye urefu wa kilometa 16, vivuko viwili vya Miguu pamoja na Makalavati
 na unatarajiwa kumalizika katika kipindi cha miezi 8 kwa gharama ya 
zaidi ya Shillingi Bilioni Moja.
Skimu ya Umwagiliaji ya Kirya ina zaidi ya wanufaika Elfu mbili (2000) wanaolima zao la mpunga na Mbogamboga.
Mashine aina ya EXCAVATOR ikichimba Mfereji Mkuu unaotoa Maji kwenye Banio hadi katika Skimu ya Kirya.
Mkurugenzi
 wa Halmashauri ya Mwanga Bi, Mwajuma Nasombe (aliyevaa Miwani) akitoa 
maelekezo kwa Bw, Nyange Laizer mjumbe wa kamati ya Ujenzi kuhusu wajibu
 wa jamii ya Kirya kutoa ushirikiano unaohitajika kwa Mkandarasi.
Wahandisi
 na Wataalam wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakitazama Banio la pili 
litakaloanza kutumika mara baada ya Mfereji Mkuu kukamilika. 

No comments:
Post a Comment